• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Madereva Bodaboda Chamwino watakaokidhi Vigezo Kutapatiwa Mikopo

Imewekwa: November 24th, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Gift Isaya Msuya amewataka madereva bodaboda kufuata sheria, taratibu na kanuni zinazowaongoza katika kazi yao na kwa kufanya hivyo wataweza kusaidiwa mikopo kwa ajili ya kununua pikipki zao wenyewe kupitia vikundi watakavyoviunda.

Ahadi hiyo ameitoa alipokuwa kwenye hafla ya kukabidhi vyeti kwa mabodaboda 171 waliohitimu mafunzo ya udereva wa pikipiki Novemba 24, 2023 ambapo alikuwa mgeni rasmi. Mafunzo yaliyotolewa na chuo cha Wide Driving Institute cha mkoani Dodoma.

Ameahidi pia kutoa leseni kwa madereva bodaboda waliohitimu mfunzo isipokuwa ameeleza kuwa wanachopaswa kufanya ni kuwa na TIN namba , namba ya NIDA pamoja na kulipia gharama za leseni, na amesema atatoa maelekezo kwa maafisa wa NIDA na TRA kutoa ushirikiano unaohitajika ili waweze kupata vitu hivyo kwa urahisi

" Ofisi ya Mkuu wa wilaya itahakikisha inawezesha upatikanaji wa leseni kwa urahisi, ofisi ya NIDA iko chini ya Mkuu wa Wilaya, lakini pia Ofisi ya TRA iko chini ya Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Wilaya ndio mwenyekiti wa kamati ya mapato ya Wilaya kwa hiyo hayo mengine ni maelekezo tu." Alisema Mkuu wa Wilaya.

Aidha amewashukuru chuo cha Wide Driving Institute kwa kukubali ombi la Serikali la kutoa mafunzo kwa bodaboda hao.

"Natoa pongezi kwa viongozi mbalimbali nikianza na chuo cha Wide Driving Intitute, baada ya Serikali kuzungumza na ninyi kuwaomba kwamba tuna clash program ya kuwanoa vijana wetu maafisa usafirishaji, tunahitaji wapatiwe elimu ya kuendesha vyombo vya moto, lakini namnaya kuzuia ajali nyigi ambazo zinatokea, waweze kupata mafunzo hayo. Hamkusita bali mlikubali kwa moyo mmoja." Alisema Mkuu wa Wilaya.

"Na gharama ilikuwa ni kubwa sana toka 75, 000/= wao walikubali kutoa kwa gharama ya 20,000/= kwa hiyo wametusaidia kwa kiasi kikubwa hii ni kazi nzuri iliyofanywa na Wide Driving Institute. Japo najua gharama hizi mmelipia wenyewe lakini najua nisehemu ya uwajibikaji maana mkilipiwa kila kitu baada ya kwenda kusoma hata ulichojifunza utaona hakina maana." Alisema Mkuu wa Wilaya.

Aliishukuru pia Ofisi ya Polisi Wilaya kupitia Mkuu wa usalama barabarani Wilaya kwa kuhakikisha mambo yote yanawezekana, ofisi ya Mkurugenzi kwa kushiriki kikamilifu kuhakikisha haya yanayofanyika leo yaweze kutokea, alimshukuru pia Mhe. Mbunge wa jimbo la Chamwino walipomfikishia wazo hili, angekuwa ni kiongozi asiyefahamu jambo hili angeweza kulipinga, lakini alikubali nakuunga mkono kwa asilimia mia moja wakishirikiana na Mhe. Diwani wa Buigiri.

Aliendelea kueleza kuwa mbunge aliahidi kuwajengea bodaboda vibanda kwa ajili ya kujikinga jua na mvua. Aliwashukuru pia LATRA.

Mkuu wa Wilaya alielekeza bodaboda kujisajili ofisi ya mkurugenzi na kuunda vituo ili wawe rasmi.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.