• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Dkt. Mpango Toa Rai Kwa Viongozi Kutambua Wajibu Wa Kutekeleza Dira Ya Taifa 2050 Na Mipango Ya Maendeleo Ya Sekta Ya Kilimo

Imewekwa: August 1st, 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa rai kwa viongozi kutambua wajibu wa kutekeleza Dira ya Taifa 2050 na mipango ya maendeleo ya sekta ya kilimo ambayo imedhamiria kuongeza kasi ya ukuaji wa kilimo hadi kufikia asilimia 10 kwa mwaka ifikapo 2030 na kuendelea.

Makamu wa Rais ametoa rai hiyo wakati akifungua maonesho na sherehe za Wakulima maarufu kama Nanenane zinazofanyika kitaifa katika viwanja vya Nzuguni Mkoani Dodoma. Amesema ni vema viongozi kuwajibika kuwaelekeza wakulima , wafugaji na wavuvi kuweka nguvu zaidi kwenye mazao yenye thamani kubwa sokoni, kuwekeza katika uzalishaji wa kisasa ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje, kuvutia uwekezaji wa ndani na nje pamoja na kuwekeza katika miundombinu baridi ya uhifadhi na usafirishaji.

Ameongeza ni vema viongozi kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika teknolojia za kisasa za kilimo, ikiwemo kilimo janja, uwekezaji katika umwagiliaji, upatikanaji wa fedha na mitaji, kutafuta masoko ya uhakika na kuhakikisha wanajiimarisha zaidi katika kilimo-biashara.

Pia Makamu wa Rais amesema ni inapaswa viongozi kusimamia uwezeshaji wa wakulima, wafugaji na wavuvi kiuchumi, hususani upatikanaji wa mitaji, teknolojia, elimu na mafunzo pamoja na upatikanaji wa huduma za ugani, ikiwemo kukuza matumizi ya kanuni bora za kilimo. Halikadhalika kuhamasisha maendeleo ya ushirika na ushirikiano kati ya wakulima, wafugaji, wavuvi na watafiti, maafisa ugani na watunga sera.

Vilevile Makamu wa Rais amesema ni wajibu wa viongozi kuhimiza Wananchi kutumia mbinu zinazoweza kuhimiri athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi na changamoto nyingine zinazowakumba wakulima ikiwemo kuhimiza matumizi bora ya ardhi, kushawishi wananchi kupanua mawanda ya kilimo na kuhimiza zaidi kilimo cha mazao yanayohimili ukame.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa viongozi kutoa elimu kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wasindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi kuhusu fursa zilizopo na kupata mitaji kutoka kwenye benki na taasisi zingine za fedha ambazo tayari zinatoa mikopo nafuu kwa ajili ya kilimo-biashara

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Dkt. Mpango Toa Rai Kwa Viongozi Kutambua Wajibu Wa Kutekeleza Dira Ya Taifa 2050 Na Mipango Ya Maendeleo Ya Sekta Ya Kilimo

    August 01, 2025
  • Wanakijiji Ndebwe, Chamwino Wapatiwa Majiko Banifu

    July 29, 2025
  • Wataalam Kutoka Mkoani Wakagua Miradi Chamwino

    July 29, 2025
  • LGTI Yakinoa Kikosi Kazi Cha Halmashauri Kupambana Na Mabadiliko Ya Tabia Ya Nchi

    July 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.