• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Wakabidhiwa Ngao Mashindano Ya Mazingira

Imewekwa: November 3rd, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kupitia mdau wake taasis ya LEAD Foundation inayoendesha mradi wa Kisiki Hai imefanikiwa kupata ushindi wa kwanza kwenye shindano lililohusu masuala ya kilimo hifadhi makinga maji na utunzaji wa vyanzo vya maji, utungaji wa nyimbo za mazingira, mchezo wa mpira wa miguu na mpira wa pete.

Mshindi wa kwanza alikabidhiwa ngao na ngao hiyo imekabidhiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji na Bi Happy Mkalawa mratibu wa mradi wa Kisiki hai Chamwino leo Novemba 3, 2023 na kupokelewa kwa niaba ya Mkurugenzi na Bibi Prudence Kaaya Ching'ole Ofisini kwake.

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo mratibu mradi wa Kisiki Hai ameeleza kuwa zipo hatua nne za kutunza kisiki hai ya kwanza ni kuchagua au kukitambua kisiki hai.

" unaangalia matawi ambayo yameshiba na yanakuwa kuelekea juu, ambayo hayana afya yanapaswa kuondolewa ili kupunguza ushindani wa chakula nà hewa." Alisema Mkalawa.

Alieleza hatua ya pili ni kupogolea ambayo ni hatua ya kuondoa matawi yasiyohitajika. Aliendelea kueleza kuwa unapopogolea unapaswa kuangalia kifaa kiwe na makali ya kutosha, makali yaelekee juu yasielekee chini ilikusudi usijeruhi mti. Mti ukipata jeraha inakuwa rahisi kukaribisha wadudu wakaushambulia.

Vilevile alieleza kuwa haipaswi kupogolea karibu na maungio angalau utoke nje kidogo ya maungi ya tawi la mti.

Mratibu alieleza pia kuwa hatua ya tatu ni kuweka alama kujulisha kuwa mti ni wa kisiki hai hivyo unatunzwa na unatambulika.

" Unapaswa kufungwa kitambaa chenye rangi yeyote ile ambayo inaweza ikatambulisha jamii kwa namna yeyote ile kuwa hiki ni kisiki hai na kinatunzwa." Alisema Mkalawa.

Hatua ya mwisho ilielezwa kuwa ni kutunza hivyo inashauliwa kuutembelea mara kwa mara ili kuona iwapo umeshambuliwa na wadudu au umevamiwa na mifugo lakini pia kama umexhipua zaidi ili uweze kuupogolea tena. Pia inashauliwa kuwa aawe amepanda mazao mengine kwenye shamba yatakayojfanya afike mara kwa mara kuangalia maendeleo ya visiki hai. Klielezwa kuwa anaweza kuwa amepanda mihogo au mbaazi.

Wilaya zilizoshiriki kwenye mashindano haya ni Chamwino kutoka mkoa wa Dodoma na Ikungi kutoka mkoa wa Singida.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.