Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wakulima na Wafugaji Chamwino Waunda Jukwaa

Imewekwa: August 4th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imefanya Mkutano maalum wa kuunda Jukwaa tendaji la Kilimo, Ufugaji na Ardhi lenye lengo la kuwakutanisha Wakulima na Wafugaji ili iwe rahisi kuwahudumia.

Mkutano huo maalum umefanyika katika ukumbi wamikutano wa Halmashauri leo Agosti 4, 2023 ambapo umeshirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na wakulima na wafugaji.

Akizungumza alipokuwa anafungua mkutano Mkurugenzi mtendaji wa Wilaya Dkt. Semistatus Mashimba amesema Jukwaa watakalounda litasaidia kuzungumzia changamoto za wakulima na wafugaji pamoja na kuzitatua.

 " ninafahamu wakulima, wafugaji wanachangamoto nyingi, lengo la jukwaahilo ni kuhakikisha sisi kama Serikali tunawakutanisha na hawa watu wanaotatua changamoto zenu. Zipo Taasisnyingi zinapiga simu ofisi ya Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya zinasema zinataka kusaidia wakulima na wafugaji na wamojawapo ni mradi wa kuwainua wanawake UN WOMEN na siyo Taasis tu hata Serikali." Alisema Mkurugenzi.

Wajumbe wameweza kuchangia mawazo yao kwenye Rasimu ya Katiba ya Jukwaa tendaji la Kilimo, Mifugo na Ardhi na wote kwa pamoja walikubali kuundwa kwa Jukwaa hilo pamojà na kupitisha rasimu ya katiba.

Uzinduzi wa Jukwaa hilo unatarajiwa kufanyika Agosti 25, 2023 kwenye Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino.

Akizungumza kwenye uundaji wa Jukwaa Mwenyekiti wa wafugaji John Kochocho amempongeza Mkurugenzi kwa maono yake ya kuanzisha Jukwaa na kuwasihi wafugaji wenzake kujiunga nalo kwani linafaida kubwa kwao.

"Nakupongeza Mkurugenzi kwa jambo ulilolifanya la kuunganisha wakulima na wafugaji kwa kuwa huwawanachangamoto sana na wanashindwa watazipitisha wapi. Ninaimani hili jukwaa wakulima na wafugaji litakuwa kimbilio lao",alisema mwenyekiti wa wafugaji.

" Sisi huwa hatuamini kitu mpaka uone mwenzako ameingia, ingia utaona faida. Faida yake kwenye kupimiwa ardhii, lakini hata kututafutia masoko ya mifugo. Hakuna mfugaji masikini, mbuzi mmoja tu kwa sasa anauzwa karibu shilingi laki moja." Alisema Mwenyekiti wa wafugaji.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya amepongeza uundwaji wa Jukwaa hilo na kusema litaondoa migogoro ya wakulima na wafugaji nakuwaomba wakulima na wafugaji kujiunga na chombo hicho kwani kiingilio wamekiweka wao wenyewe.

" Tunapozungumzia migogoro ya wakulima na wafugaji tuliyonayo hiki chombo ndio kitakwenda kuimaliza", alisema Mwenyekiti.

Vilevile amezielekeza taasis za benki hususani NMB kuona ni namna gani watatoa mikopo kwa wakulima na wafugaji watakaokuwa wamepimiwa ardhi zao na TRA baadae Jukwaa litakapoanza waeleze ni kwa namna gani watasajili mifugo na wakulima ili wawezkupata mikopo kwenye vyombo vya kifedha.

Wadau waliosaidia katika shughuli ya uundwaji wa Jukwaa ni pamoja na UN WOMEN, NMB Benki, CRDB Benki, TOAM, PBZ Benki

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chamwino Yaweka Mikakati Kuhakikisha Wanafunzi Wanamaliza Mzunguko Wa Elimu

    May 28, 2025
  • Wamiliki Mashine Za Kusaga Nafaka Wahimizwa Kufunga Vinyunyizi Vya Virutubisho

    May 26, 2025
  • Mchengerwa Awataka Maafisa Habari Kuhakikisha Wananchi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Miche 350 Ya Matunda Yapandwa Kuadhimisha Kampeni Ya "Mti Wangu Birthday Yangu"

    May 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.