• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru Wapitisha Miradi Yote Iliyotembelea Chamwino

Imewekwa: October 6th, 2023

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023 ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Chamwino kwa kusimamia vizuri miradi ya maendeleo ambayo Mwenge wa Uhuru  umefika na kujionea shughuli ambazo zimefanywa na kukuta zimekamilika kwa wakati.

Pongezi hizo amezitoa kwa mkuu wa wilaya ya Chamwino Mhe.Gifty Isaya Msuya pamoja na viongozi wote wa wilaya ya Chamwino kwa kushirikiana vizuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyopo wilayani hapa.

Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2023 umefanya ukaguzi wa nyaraka mbalimbali, kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo na kujionea juu ya ubora na viwango vilivyozingatiwa pamoja na kuangalia thamani ya matumizi ya fedha kama  inaendana na maendeleo ya miradi iliyopo wilayani Chamwino.

Mwenge wa Uhuru ambao bado  uko Mkoani Dodoma  ulifika katika Wilaya ya Chamwino siku ya tarehe 04.10.2023 ambapo Mwenge huo wa Uhuru ulipokelewa kutoka wilaya ya Dodoma na makabidhiano hayo yalifanyika baina ya wakuu wa wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri na Mhe. Gifty Isaya Msuya.

Baada ya kupokelewa kwa Mwenge huo ulitembelea Miradi mbalimbali ikiwemo Miradi ya Maji na Elimu, kutembelea na kujionea vijana wa kikundi cha ELLYDIZDON wanavyofanya kazi za uzalishaji na utengenezaji bidhaa mbalimbali pamoja na kutembelea shamba linalolimwa kwa kutumia kilimo cha kisasa la Mwekezaji wa kilimo David Mwaka ambalo lina ukubwa wa hekta 40 (Mtimbi Farm).

Mbali na Mwenge wa Uhuru kutembelea miradi hiyo ulipita katika Hospitali ya Uhuru iliyopo wilaya ya Chamwino na kutembelea mabanda mbalimbali yalyokuwa yakitoa Elimu za Lishe, Rushwa, Ukimwi, madawa ya kulevya na malaria.

Sanjari na hayo pia Mwenge wa Uhuru ulitembelea Mradi wa Uhifadhi wa Mazingira katika kitalu cha Miti Ikowa ambapo wakimbiza Mwenge Kitaifa na viongozi mbalimbali walipata fursa ya kupanda Miti katika Eneo Hilo.

Mwenge wa Uhuru umepitisha miradi yote ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino baada ya Miradi yote kukidhi vigezo vya ubora unaotakiwa.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.