• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mayanja Atoa Rai Uchangiaji Chakula Shuleni

Imewekwa: August 29th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja amewaelekeza wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kusimamia suala la wanafunzi kula chakula shuleni. Hayo ameyasema kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani wa mwaka uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Agosti 28,2024.

"Agenda ya chakula shuleni iwe ya kudumu kwenye mikutano yenu mnayofanya na wananchi, na tuwaelimishe wazazi na walezi chakula wanachokula shuleni ni kilekile ambacho mtoto angekula akiwa nyumbani." Alisema Mhe. Mayanja.

"Kuna wazazi wenginewanaona kama Chakula wanachokula shuleni ni kama anakula na watu wengine. Nadhani eneo hilo linahitaji elimu kwa sababu mtoto akila chakula shuleni inaweza kumuongezea ufaulu. Naomba tuwaelimishe wananchi." Alisema Mkuu wa Wilaya.

Mkuu wa Wilaya pia ameongelea suala la changamoto ya uvamizi wa simba ndani ya Wilaya na na kwamba Serikali imeshachukua hatua ya kukabiliana nao.

"Tulipata changamotomya simba kwenye jata ya Ikowa, Msamalo, Manchali, Majeleko na sasa Chilonwa. Simba wale wamekuwa wakitoka kata moja kwenda kata nyingine. Kuna simba wawili wanaonekana wapo kwenye maeneo yetu. Serikali imeshachukua hatua, kikosi cha TAWA kiko hapa na TAWIRI wanafanya kazi ya kuhakikisha kwamba simba hawa wanaondoka katika maeneo yetu." Alisema Mkuu wa Wilaya.

Kwa upande wake Mhe. Edison Sweti Mwenyekiti wa Halmashauri ameeleza kuwa wameshakaa na wahe. Madiwani kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ya jinsi ya kujikinga na wakati huohuo askari wa wanyama pori wapo kwenye maeneo hayo ambayo simba wanaendelea kuzunguka, na tunashukuru simba hao tangu wameanza hawajamdhuru mwananchi yeyote ila tu wanadhuru mifugo ng'ombe na mbuzi.

Wakati huohuo mkutano mkuu umefanya uchaguzi wa Mkamu mwenyekiti wa Halmashauri ambapo kikanuni hufanyika kila baada ya kumaliza mwaka wa fedha na Mhe. Keneth Yindi amechaguliwa tena kuwa Makamu Mwenyekiti kwa mwaka huu wa fedha kwa kupata 100% ya kura za ndiyo ya kura zote zilizopigwa na wajumbe kutokana na kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.