• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Elimu Tahadhari Ugonjwa Mpox Yatolewa Chamwino

Imewekwa: August 28th, 2024

Waheshimiwa Madiwani wamepatiwa elimu kuhusu ugonjwa wa mlipuko wa homa ya MPOX ambayo tayari imeshazikumba baadhi ya nchi za Afrika Mashariki kama vile Kenya na Burundi kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani robo ya nne ya mwaka wa fedha 2023/2024 uliofanyka ukumbi wa mikutano wa Halmashauri Agosti 27, 2024.

Akizungumza kwenye kikao hicho Dkt. Sophia M. Nchimbi mratibu wa tiba, dharura pamoja na maboresho Halmashauri ya Chamwino amesema ugonjwa huo unatokana na virus vya monkeypox ambavyo vinapatikana kwenye wanyama jamii ya nyani na wanyama wengine kama paka na panya.

Daktari alieleza njia zinazotumika kuambukiza ugonjwa huo ikiwemo kula kitoweo ambacho hakijaaiva vizuri chenye kutokana na nyama pori jamii hiyoau kugusana nao au kushika kinyesi chao, kushika majimaji au kushikana na mgonjwa, nguo, vyombo na vitu vingine vilivyotumika na mgonjwa wa Mpoxi pamoja na kujamiiana na mtu mwenye ugonjwa huo, kubusiana.

Dalili za ugonjwa imeelezwa kuwa ni kutoka malengelenge au vipele kama tetekuwanga, uchovu wa mwili, maumivu ya mgongo, maumivu ya misuli, kuvimba mitoki ya mwili, vidonda vya koo, maumivu ya kichwa pamoja na homa.

Amewataka Wahe. Madiwani wasaidie kuwaelimisha wananchi kuhusu ugonjwa huu jinsi unavyoambukiza pamoja na jinsi ya kujikinga ambapo ameeleza kuwa wananchi wanapaswa kunawa mikono vizuri kwa kutumia sabuni na maji tiririka pamoja na vitakasa mikono. Vilevile kuepuka vitu vinavyoweza kusababisha maambukizi.

Aidha Daktari ameelekeza waweze kutoa taarifa pindi wanapoona mtu mwenye dariri za ugonjwa na pia awahishwe sehemu ya kutolea huduma za afya.

Vilevile Serikali Wilayani Chamwino imeahidi kutoa mbegu za ruzuku kwa wakulima kwa msimu wa kilimo wa 2024/2025 mapema mwanzoni mwa msimu pamoja mbolea ya ruzuku.

Hayo yameelezwa na mkuu wa Idara ya Kilimo na mifugo wa Wilaya Ndg: Godfrey Mnyamale alipokuwa akijibu swali la Mhe. Diwani wa Majeleko Musa Omary aliloliuliza kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani akihofia mbegu kuchelewa kutolewa kwa mbegu kunakoweza kupelekea wakulima kuchelewa kupanda na hivyo kupata mavuno hafifu.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.