• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Yapata vikombe Vitatu Mashindano ya UMISSETA

Imewekwa: June 8th, 2019

Chamwino Yanyakua vikombe Vitatu Mashindano ya UMISSETA

Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imejinyakulia vikombe vitatu baada ya kushika nafasi ya kwanza katika mashindano ya UMISSETA ngazi ya Mkoa.

Vikombe hivyo vimekabidhiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji Wilaya Ndugu Athumani H. Masasi na Afisa Elimu Sekondari Ndugu David Mwamalasi Ofisini kwake mapema wiki ambapo nae alivikabidhi kwa Mwenyekiti wa Halmashauri Ndugu Samwel A. Kaweya.

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi vikombe hivyo Afisa Elimu Sekondari alisema, “Chamwino imeshinda nafasi ya kwanza katika michezo ya mpira wa pete (netball), mpira wa wavu(volleyball) wasichana na sanaa za maonyesho (ngoma).”

Aliendelea kueleza kuwa Wilaya pia imefanikiwa kupata ushindi wa pili kwa michezo ya mpira wa miguu (football), mpira wa kikapu(basketball) na mpira wa wavu ( volleyball) wavulana ambapo walizawadiwa vyeti kwa kushika nafasi hiyo ya pili.

Vilevile alieleza kuwa Wilaya imefanikiwa kushinda mchezo wa Riadha mita 100 na 800 Wavulana.

Aidha katika taarifa yake alisema kuwa Wilaya imefanikiwa kupeleka uwakilishi wa wanamichezo ishirini na tano (25) kati ya mia moja (100) waliochaguliwa kuuwakilisha Mkoa ngazi ya Taifa.

Kati yao riadha wavulana wawili, mpira wa miguu wavulana wawili, mpira wa pete wasichana wanne (4), mpira wa kikapu wavulana wawili (2) na mpira wa wavu wavulana mmoja (1) na kikundi cha ngoma jumla ya waimbaji 14.

Ushindi huo umepokelewa kwa furaha kubwa na viongozi wote. Wakiongea kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wamewataka Wataalam kuhakikisha wanafanya vizuri kwenye Nyanja zote na si kwenye michezo tu.

Mkurugenzi Mtendaji Wilaya pia alitimiza ahadi yake aliyoitoa kwa wanamichezo ya kutoa shilingi 200,000/= kwa kila kikombe watakachokipata katika mashindano hayo ya ngazi ya Mkoa kama motisha kwa wanamichezo hao.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chamwino Waibuka Kidedea Tuzo Za MSD Kanda Ya Kati

    May 11, 2025
  • Kata, Shule Na Walimu Walioibuka Kidedea Kwa Ufaulu 2024 Wajizolea Vitita Chamwino

    May 10, 2025
  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.