• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Yaazimisha Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar Kwa Kutoa Sare za Shule

Imewekwa: January 12th, 2024

Leo Januari 12, 2024 ikiwa ni siku ya Maadhimisho ya Miaka sitini (60) ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Timu ya Itifaki wilaya ya Chamwino (Protocol service Team) PST Kwa kushirikiana na Taasisi ya PTO (Tanzania Patriotic organisation) wamezindua kampeni maalumu waliyoipa jina la" Nirudishe shuleni"  ya kuwapatia mahitaji na vifaa vya shule wanafunzi wenye uhitaji mashuleni ili waweze kutimiza ndoto zao za kielimu.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa PST ndugu Hussein Hussein wakati akizingumza katika zoezi Hilo lililofanyika katika shule ya Msingi Buigiri wasioona (Buigiri blind school) iliyopo kata ya Buigiri wilaya ya Chamwino ambapo wameanza kwa kugawa sare za shule kwa wanafunzi 100 wa shule hiyo.

"Kwakuwa PST ni Taasisi inayoaminika katika kusimamia shughuli mbalimbali za kiitifaki  za Serikali na kupitia wazo la Mkuu Wa wilaya ya Chamwino ndugu yetu GIFT MSUYA tumekuja na kampeni hii inayolenga kuwashika mkono wanafunzi wenye uhitaji na Leo Kwa umuhimu mkubwa tumeona tuanzie katika shule hii ya Buigiri kwakuwa ni nyumbani, huu ni mwanzo tu lakini tunatarajia kuzifikia shule 84 , pia niwaahidi wanafamilia ya Buigiri wasioona tutaendelea kuja zaidi ili kutoa vifaa mbalimbali vya shule kadri vitakavyohitajika." Alisema Hussein.

Kwa upande wake Mgeni Rasmi ambaye pia ni  Mheshimiwa Diwani Wa  kata ya Buigiri Kenneth Yindi amewapongeza PST na PTO Kwa kutambua umuhimu Wa kufanya zoezi Hilo la kizalendo kwa kusherehekea Maadhimisho ya Mapinduzi, akieleza kuwa kila mtanzania anapaswa kuwa mzalendo katika nafasi yake ili kuhakikisha ustawi wake na Taifa kwa ujumla. Pia Ametoa Wito Kwa Wananchi kusaidiana, kupendana ,kuthaminiana na kutoa taarifa za uharibifu Wa Mali za umma ama wizi unaotokea kwenye maeneo yetu katika Mamlaka husika Kama sehemu ya uzalendo.

Naye Katibu Tawala wilaya ya Chamwino Neema Nyarege ambaye pia amemwakilisha Mkuu Wa wilaya Mheshimiwa Gift Msuya katika hafla hiyo, ametumia fursa hiyo kueleza kuwa lengo la Mheshimiwa Msuya kuwashauri PST Kuja na kampeni hiyo ni jema , hivyo ofisi ya Mkuu wa wilaya iko tayari kuwaunga Mkono wakati wote ili waweze kutimiza Adhma ya kuwarudisha watoto shule Kama kampeni Yao inavyojieleza. Pia amesema mlango uko wazi Kwa Taasisi yeyote inayohitaji kufanya shughuli za kijamii na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ipo tayari kushirikiana nao.

Tukio Hilo ambalo awali limetanguliwa na zoezi la upandaji Miti katika viunga vya shule hiyo, limehudhuriwa na katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chamwino, viongozi wa CCM kata ya Buigiri, viongozi wa Serikali kata ya Buigiri, kaimu Afisa Elimu msingi Wilaya, Katibu wa Mbunge jimbo la Chamwino, wanafunzi wa shule ya sekondari Chamwino na jumuiya ya shule ya Msingi Buigiri wasioonana.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.