Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Waziri Bashe Akagua Miradi Mikubwa ya Kilimo, Chamwino

Imewekwa: September 29th, 2022

" Nimeridhishwa na mradi unavyoendelea, kazi iliyofanyika ni nzuri".

Maneno haya yamesemwa na Waziri wa Kilimo Mhe. Hussen Bashe alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya kilimo Wilayani Chamwino Septemba 28, 2022.

Miradi iliyokaguliwa ni mradi wa kilimo cha zabibu Chinangali na mradi wa ujenzi wa Bwawa la umwagiliaji Membe.

Katika miradi yote miwili Mhe. Bashe ameridhishwa na kazi inavyoendelea na ametoa maelekezo mbalimbali kwa wasimamizi wa miradi hiyo.

Kwenye mradi wa shamba la zabibu Chinangali wenye ekari 600, ameelekeza wakulima waliopo kwenye eneo lililobaki jirani na shamba hilo waorodheshwe  na maeneo yao yaingie kwenye mradi huu ili wapate walau ekari 1000 kwa ajili ya kilimo cha mashamba makubwa( block farming).

Mhe. Waziri pia ameeleza adhima ya Serikali ya kujenga kiwanda cha kuchakata na kutengeneza mchuzi wa zabibu ambapo wakulima wataongeza thamani ya zao hilo nakuuza kwa bei nzuri kuliko wanavyouza sasa ikiwa ni pamoja na kuwa na soko la uhakika.

' Tukifanikiwa kujenga kiwanda maana yake wakulima watauza mchuzi wa zabibu. Kilo moja ya zabibu kwa sasa ni shilingi elfu moja lakini lita moja ya mchuzi wa zabibu ni shilingi elfu tatu, hivyo mkulima ataondokana na adha ya kukosa soko. Halmashauri pia itaweza kupata ushuru mzuri ( produce cess). Alisema Mhe. Waziri.

Naye Mwenyekiti wa chama cha ushirika cha CHABUMA AMCOS ndugu David Mwaka ameeleza kuwa kazi ya kusafisha shamba inaendelea vizuri, tayari wamesafisha kwa 99% na kazi ya kusambaza drippers inaendelea. Amemuomba Mhe. Waziri wazo lake la kujenga kiwanda alifanyie kazi kunusuru soko la zabibu. 

" Mwaka huu zabibu nyingi zimeharibikia shambani tunakuomba lile wazo lako la kujenga kiwanda ulifanyie kazi kunusuru soko la zao la zabibu". Alisema Mwenyekiti wa CHABUMA AMCOS.

Akiwa kwenye mradi wa ujenzi wa bwawa Membe, Mhe. Waziri amempongeza Mkandarasi kwa kazi nzuri.

Vilevile Mhe. Bashe ametoa maagizo kwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kupitia upya na kuorodhesha wakulima wanaolima kwenye eneo la mradi wa Membe ili wapewe maeneo na eneo linalobaki litagawiwa kwa vijana. 

"Naagiza Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji mfanye upya mapitio ya wakulima wanaolima kwenye eneo la mradi ili tuwatambue na kuwagawia maeneo kama ni ekari 5 au 10 ili asije kuibuka mtu na kusema eneo lake limechukuliwa, na kisha eneo linalobaki tutaligawa 9kwa vijana. Tunataka kilimo chenye tija na kuondokana na ukulima mdogomdogo wa kujikimu". Alisema Mhe. Bashe.

Vilevile Mhe. Waziri ameelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kukaa na vyama vya ushirika na kufanya tathimini ya mavuno kwa wakulima wadogo waliokopeshwa fedha na benki ya CRDB ili kuona ni kiasi gani kinaweza kulipika na kwa wale ambao hawakuwa na mavuno mazuri  waorodheshwe walipe kwa msimu ujao wa 2022/2023.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Ashiriki Zoezi La Kuboresha Taarifa Kwenye Daftari La Kudumu La Wapiga Kura

    May 17, 2025
  • Mafunzo Ya Uboreshaji Wa Daftari La Wapiga Kura Awamu Ya Pili Yatolewa Chamwino

    May 14, 2025
  • Chamwino Waibuka Kidedea Tuzo Za MSD Kanda Ya Kati

    May 11, 2025
  • Kata, Shule Na Walimu Walioibuka Kidedea Kwa Ufaulu 2024 Wajizolea Vitita Chamwino

    May 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.