• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Huduma Za Afya Zazidi Kuimarika Chamwino, Hospitali Ya Wilaya Na Zahanati Nne Zapata Neema

Imewekwa: October 11th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja, leo Oktoba 10, 2025 amekabidhiwa na taasisi ya ELICO vyombo vya usafiri, na vifaa mbalimbali vya TEHAMA; ikiwa ni pamoja na pikipiki tatu za umeme, baiskeli moja ya umeme, kompyuta tatu, printa tatu na vifaa vya kutunza umeme (UPS) tatu kwa ajili ya zahanati ya Chitabuli, Chiwondo, Mafurungu, na Mahamha.

Akizungumza wakati wa makabidhiano yaliyofanyika katika zahanati ya Mahamha, Mhe. Mayanja amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya ELICO Ndg. Sisty Basil kwa kuona haja ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya katika Wilaya ya Chamwino.

“Tunakushukuru kwa kuichagua Wilaya ya Chamwino, kwani mngeweza kuchagua wilaya nyingine yoyote ya mkoa wa Dodoma, lakini imewapendeza kuichagua wilaya ya Chamwino, na kuunga juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya katika Wilaya hii.”

Vilevile Mhe. Mayanja amempongeza Kaimu Mkurugenzi na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Dkt. Euseby Kessy, kwa namna ambavyo anafanya kazi na wadau wa maendeleo hasa taasisi zisizo za kiserikali zinazojitokeza kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya katika wilaya ya Chamwino.

Kadhalika, Dkt. Kessy ameshukuru taasisi ya ELICO kwa kuanzisha ushirikiano na serikali, na kuwezesha upatikanaji wa vitendea kazi mbalimbali katika sehemu za kutolea huduma za afya, hasa zahanati mpya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mganga Mfawidhi wa zahanati ya Mahamha Dkt. Martin Dorothei Mluge na Mganga Mfawidhi wa zahanati ya Chiwondo, Dkt. Lucy Mushi  wamesema kwamba kuwepo vitendea kazi hivyo kutaboresha huduma za afya katika zahanati zao hasa huduma ya mkoba  na utunzaji wa taarifa.

Mbali na vifaa vilivyokabidhiwa leo, taasisi ya ELICO imejenga visima vya maji vitatu, ikiwa ni kimoja kimoja katika hospitali ya Wilaya ya Chamwino, Zahanati za Chitabuli na Mafurungu, pamoja na kuvifungia pampu zinazotumia umeme wa jua. Pia, taasisi hiyo imefunga mifumo ya umeme wa jua katika zahanati zote nne ambazo ni wanaufaika wa vitendea kazi vilivyokabidhiwa leo.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Huduma Za Afya Zazidi Kuimarika Chamwino, Hospitali Ya Wilaya Na Zahanati Nne Zapata Neema

    October 11, 2025
  • Wanufaika Wa Miradi Ya Maendeleo Chamwino Watakiwa Kuitunza

    October 03, 2025
  • Mwenyeķiti Wa INEC Jaji Wa Rufani Jacobs Mwambegele Atembelea Ghala la Vifaa Vya Uchaguzi Chamwino

    September 25, 2025
  • RAS Dodoma Afanya Ziara Ya Kujitambulisha Chamwino, Atoa Maelekezo Kwa Halmashauri

    September 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.