• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi Chamwino Kupata Soko La Uhakika la Zabibu

Imewekwa: April 19th, 2024

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Staki Senyamule leo April 20, 2024 amefanya ziara ya kikazi Wilayani Chamwino na kukagua miradi na kusikiliza kero za wananchi.

Kkuhusu kero ya ukosefu wa soko la zabibu na ombi la kuwa na bodi ya zao la zabibu ilielezwq kuwa kwa sasa Serikali inakamilisha ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza mchuzi wa zabibu ambapo kitakapokamilika kitaondoa tatizo la kuharibika kwa zabibu.

"Kumekuwa na changamoto kubwa sana ya soko la zabibu ambalo l8mekuwa likiwasumbua sana wakulima wa zabibu, jambo ambalo Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia ililiona hili. Pale kwenye shamba la Chinangali tunajenga kiwanda cha Serikali ambacho kitakuwa kinauwezo wa kuwahudumia wananchi wote walioko kwenye maeneo ya Mvumi misioni, Mvumi Makulu, Makang'wa, Handali pamoja Nghahelezi wenye zabibu nyingi." Alisema Godfrey Mnyamale.

"Kiwanda kile kipo kwenye hatua za mwisho za ujenzi, mkandarasi anatarajiwa kuingiza mitambo mwezi wa tano, tunatarajia kwa hatua za awali tunaweza kupata zabibu za kwanza za mwezi wa tisa ziingie kwenye kile kiwanda." Alisema Mnyamale

Kuhusu suala la Bodi ya zabibu mkuu wa Idara ya kilimo ameeleza suala hili linashughulikiwa na Mrajisi wa ushirika na wameanza hatua ya kwanza ya kutengeneza chama cha ushirika. Amewaomba wakulima waendelee kuiamini Serikali na tunaamini baada ya muda mfupi changamoto ya masoko ya zqbibu itakuwa imeondoka.

Akizungumza kwenye mkutano huo wa hadhara Mkuu wa mkoa alieleza kuwa kazi ya Serikali ni kuwatafutia wananchi masoko. Alimpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan k2a kutoa kipaumbele kwa sekta binafsi kutambuliwa na kutengeneza mazingira mazuri ili kuweza kujiletea maendeleo bila vikwazo.

Kuhusu ulimaji wa zabibu niendelee kuwahimiza kwani ukombozi huo unakuja wa soko la uhakika wa kuuza mchuzi au zabibu yetu katika njia ya mchuzi na kufanya tusipate shida tena. Hiyo itakuwa ni historia kwa sababu Rais wetu ameweka kipaumbele kwenye suala la uchumi. Najua asilimia 90 ya wanaChamwino wanategemea kilimo. Tukiweza kufanya mapinduzi ya kilimo basi tutakuwa tumebadilisha uchumi wa mtu mmojammoja. Alisema Mkuu wa Mkoa.

Vilevile Mhe. Senyamule aliweza kuzungumzia kuhusu utalii wa kiutamaduni wa ngomq za asili na kuwasisitiza wananchi kuutangaza ulimwenguni na kuuenzi hususani ngoma za kigogo pamoja na nyimbo za kigogo ili wanaofanya utamaduni huu waweze kuinuka kiuchumi kupitia hizo.

Utalii mwingine aliouhimiza Mkuu wa mkoa ni utalii wa zabibu ambayo kwa Tanzania inalimwa Dodoma pekee na kwa Afrika mashariki pia.

"Watakuja watu kwenye mkulima mwenye shamba bora wamlipe pesa ili walitembelee na kuwaelezea unavyolima, unavyopanda na kuvuna. Alisisitiza wakulima walime kwa ubora ili iwe kivutio siyo tu kwa kuuza bali oia kwa utalii." Alisema Mkuu wa mkoa.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.