• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

VIONGOZI CHAMWINO WAKASIRISHWA NA UNYANYASAJI WA WATOTO

Imewekwa: June 15th, 2019

Mwaka 1991, wakuu wa nchi wanachama wa umoja wa Afrika OAU walianzisha siku ya mtoto wa Afrika kama kumbukumbu ya uasi dhidi ya wnafunzi Juni 16, 1976 huko Soweto Afrika Kusini. Wakati huo, wnafunzi watoto wadogo waliandamana, kwanza kupinga aina ya elimu duni ya kibaguzi iliyotolewa na serikali ya makaburu. Pili waliitaka serikali ya makaburu iwape ruksa kufundishwa kwa lugha zao asili. Katika maandamano hayo serikali ilitumia nguvu kuwatawanya watoto waliokuwa wakiandamana na kupelekea vifo vya watoto Zaidi ya elfu mbili.

Halmashauri ya wilaya Chamwino imeazimisha imefanya maadhimisho ya kiwilaya jumamosi ya tarehe 15, Juni 2019 kwenye viwanja vya shule ya msingi Buigiri Blind. Maadhimisho hayo yaliwaleta pamoja  watoto kutoka maeneo mbalimbali  na kuto fursa kwao kueleza changamoto  mbalimbali wanazokumbana nazo katika malezi ngazi ya familia na jamii wanazotoka.

Miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili jamii ya Chamwino ni pamoja na ndoa za utotoni. Hapo mchungaji wa kanisa la Agape-Kawawa alitoa ushuhuda alivyosaidia kuzuia ndoa ya mtoto mwenye umri mdogo na ukinzani na vitisho alivyovipata kutoka katika familia iliyotaka kumuozesha mtoto.

Bw. Lucas Manyala mgeni rasmi aliyemwakilishi wa mkuu wa wilaya ameitaka jamii ya Chamwino kuhakikisha watoto wanapata haki zao za msingi na mahitaji ya msingi ikiwa ni pamoja na mahitaji yao ya msingi. Pia amewataka kutafakari kauli mbiu ya mwaka huu; “Mtoto ni Msingi wa Taifa Endelevu: Tumtunze, Tumlinde na Tumuendeleze.”  Bw Manyala amesema kuwa kauli mbiu hii inaweka msingi mkuu kwa ustawi wa mtoto.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Buigiri ndugu Kenneth Yindi akishirikiana na ofisi ya mkuu wa wilaya wameahidi kununua baiskeli kwa binti anayepata adha ya kusafiri umbali mrefu kwenda shuleni.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari ya wilaya ya Chamwino Bw. Godfrey Nyamale amesema kuwa halmashauri haipo tayari kuona unyanyasaji wa watoto ukiendelea na amewashukuru wadau wa haki za watoto Bi. Rose Zakayo wa KATUKA Paralegal Organization na Bw. Petro Nziku wa Kituo cha Amani, Haki na Msaada wa Sheria kwa kuendelea kushirikiana na Halmashauri ya Chamwino.

Nao wadau wa Haki za watoto wamefungua milango zaidi kwa watoto wa Chamwino kutoa taarifa kwao wakati wote wanapokumbana na unyasaji na kuwataka watoto wajiamini kwani sharia zipo na zitawalinda.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.