• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Atatua Kero Chamwino

Imewekwa: November 11th, 2022

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Sitaki Senyamule amefanya ziara ya kikazi wilayani Chamwino, Novemba 10, 2022 kwa lengo la kuzungumza na viongozi mbalimbali ngazi ya wilaya pamoja na watumishi na kukagua miradi ya maendeleo.

Akiwa kwenye kikao na viongozi hao pamoja na watumishi kilichofanyika kwenye jkumhi wa mikutano wa Halmashauri Mkuu wa Mkoa alipokea kero mbalimbali na zote zilipatiwa majibu.

Hoja zilizowasilishwa na kupatiwa majibu ni pamoja na soko la zabibu kusuasua na kuwa na bei ya chini na baadhi ya wakulima kutolipwa fedha zao mpaka sasa, ambapo majibu yalitolewa kuwa Serikali imeshaanza kulitafutia ufumbuzi suala la soko la zabibu.

Ilielezwa kuwa kwa mwaka huu wa fedha Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kujenga kiwanda kwa ajili ya kukamua mchuzi wa zabibu ikiwa ni pamoja na kujenga matenki ya kuhifadhia mchuzi wa zabibu suala ambalo litapunguza adha hiyo.

Kuhusu suala la wakulima kutolipwa fedha zao ilielezwa kuwa tayari kampuni ya jambo wanaendelea kulipa na walichelewa kulipa kutokana na suala hilo la kununua kutokuwa kwenye mpango wao wa bajeti isipokuwa walifanya hivyo baada ya kuombwa na Serikali kununua zabibu ili kunusuru zisiharibikie shambani.

Kero nyingine ilikuwa ni kuhusu bwawa la Manchali ambalo limechimbwa tangu mwaka 1997 na tangu kipindi hicho halijawahi kufanyiwa ukarabati na tayari limejaa mchanga na kufanya shughuli za umwagiliaji kushindwa kufanyika.

Akijibu hoja hiyo Mkuu wa Idara ya Kilimo ndugu Godfrey Mnyamale alieleza kuwa bwawa hili limeshaandikiwa maandiko na WFP walielekeza uongozi wa kata kutunza mazingira ya bwawa na kutoruhusu mifugo kuingia na kuchunga kwenye eneo la bwawa na iwapo hayo yatatekelezwa kwenye bajeti ya 2023/2024 wataleta fedha kwa ajili ya kurikarabati.

"Wameshaandika maandiko, WFP walielekeza uongozi wa kata kusimamia kutunza mazingira ya bwawa na kutoingiza mifugo na bajetimya 2023/2024 wataleta fedha.' Alisema Mnyamale.

Kuhusu kero ya daraja la Chilonwa ambalo limesababisha ajali nyingi kipindi cha masika, afisa kutoka TANROAD alieleza kuwa kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha wa 2022/2023 Serikali imetenga fedha kwa ajili ya usanifu na kazi hiyo ya usanifu ambayo inatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Februari 2023, watatangaza tenda ya ujenzi wa daraja.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bibi Fatuma Mganga ameipongeza Halmashauri kwa kupata mradi wa bwawa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na ameielekeza Halmashauri kuweka mipango mizuri ili kuongeza mapato.

"Nawapongeza kwa kupata fursa za mabwawa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji. Natarajia katika mradi wa bwawa mlioupata mipango iwe mizuri ili kuongeza mapato."Alisema Katibu Tawala Mkoa.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.