• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mhe. Dkt. Mpango Ahimiza Wananchi Kuchangamkia Fursa Za Mazao Mapya Dodoma

Imewekwa: August 22nd, 2024

MHE.DKT PHILIP MPANGO AHIMIZA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA ZA MAZAO MAPYA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Philip Isdor Mpango amesisitiza wananchi kuchangamkia fursa za mazao mapya yanayostawi vizuri katika ardhi ya Dodoma na kuachana na dhana ya mkoa wa Dodoma ni nusu jangwa kwani mkoa huo umebarikiwa kuwa na kiasi kikubwa cha maji.

Akizungumza wakati akihitimisha ziara ya siku nne mkoani Dodoma katika mkutano wa hadhara Mpwayungu wilayani Chamwino Agosti 22, 2024, amesema mazao hayo mapya ya mitende, mizeituni, komamanga, karanga za miti na parachichi kuwa ni fursa adhimu kwa wananchi kujikwamua kiuchumi na kupunguza uagizaji wa baadhi ya mazao hayo kutoka nje ya nchi ikiwemo zao la tende. Hata hivyo, amesisitiza pia fursa katika kilimo cha kimkakati cha zabibu, alizeti, mbogamboga na mpunga.

Aidha, Mh. Dkt Philip Mpango ameweka jiwe la msingi katika mradi wa kilimo wa jenga kesho iliyobora (BBT) na kuwapongeza wananchi na viongozi wa vijiji vya Mlazo na Ndogowe wilayani Chamwino kwa kutoa ardhi ya ujenzi wa mradi huo mkubwa wa skimu ya umwagiliaji iliyopewa jina la  Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pia wizara ya kilimo imesisitizwa kuhakikisha jamii ya wafugaji nayo inanufaika na mradi huo mkubwa wa umwagiliaji pamoja na kuitaka wizara ya mifugo kuanzisha mradi wa jenga kesho iliyobora (BBT) kwa wafugaji kwa kutengewa eneo na kuwekewa miundombinu ya malisho.

Kwa upande wa Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mh. Mary Prisca Mahundi (mb) ameeleza wizara hiyo kuwa mbioni kutekeleza ujenzi wa miradi mikubwa ya kuboresha mawasiliano nchi nzima na  kwa mkoa wa Dodoma minara mingi ya mawasiliano kujengwa ikiwemo wilaya ya Chamwino ambayo itanufaika na ujenzi wa minara 50.

Mh Naibu Waziri pia amempongeza mkuu wa wilaya ya Chamwino Mh. Janeth Mayanja kwa kushirikiana vyema na wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwaajili ya ujenzi wa minara katika maeneo ya Chiboli, Mlowa Bwawani na Ilangali wilayani Chamwino.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.