• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mayanja Aongoza Kikao Cha Baraza La Wafanyabiashara Chamwino

Imewekwa: October 24th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja ameongoza kikao cha robo ya kwanza cha Baraza la Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino leo tarehe 24 Oktoba, 2024 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.1

Akichangia hoja ya ujenzi wa soko na stendi ya magari katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Wilaya ya Chamwino Bw. Richard Mmasi, ameshauri wataalam wanaoratibu ujenzi wa mradi huo kuhakikisha soko na stendi vinajengwa sehemu moja ili kuvutia watu wengi zaidi ambapo itasaidia kuwa na mzunguko mkubwa wa biashara na kuleta tija na hoja hiyo iliungwa mkono na wajumbe katika baraza hilo.

Akiunga mkono hoja hiyo ya ujenzi wa soko na stand, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja ameshauri mradi huo licha ya kujengwa mahala pamoja lakini pia kujengwa karibu na makazi ya watu ili kuondoa kero ya Wananchi kufuata huduma hizo za soko na stand kwa umbali mrefu ambapo itasaidia mradi huo kuwa na tija kwa kupata watumiaji.

Sanjari na hilo, Mhe. Mayanja ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao cha baraza hilo amewapongeza wajumbe waliohudhuria kikao hicho kwa kutoa ushauri na mapendekezo yenye manufaa zaidi kwa wananchi wa Wilaya ya Chamwino.

Aidha, Katibu wa kikao hicho na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Ndg. Tito .P Mganwa amewahakikishia wafanyabiashara kuwa zoezi la upimaji wa ardhi linaendelea kwa kupima maeneo ya vipaumbele kwa ajili ya makazi , viwanda na biashara ili kuwa na mji uliopangwa na kuepuka ujenzi holela.

Kwa upande wa Afisa Biashara wa Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomola, amepongeza hali ya kuimarika kwa mabaraza ya wafanyabiashara mkoa wa Dodoma tofauti na yalivyokuwa huko nyuma, sambamba na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua umuhimu wa sekta binafsi katika kukuza uchumi wa nchi. 

Aidha, amewasihi wafanyabiashara kuchangamkia fursa za utalii zinazopatikana katika Wilaya ya Chamwino ikiwemo historia muhimu ya vijiji vya ujamaa vilipoanzishwa katika Wilaya ya Chamwino ambapo itavutia watu wengi kuja kujifunza na kukuza utalii.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.