• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi Chamwino Yapewa Maelekezo ya Kudhibiti Corona.

Imewekwa: March 19th, 2020

Kamati ya Huduma ya Afya  ya Msingi  Chamwino Yapewa Maelekezo ya Kudhibiti Corona

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Bibi Vumilia Nyamoga ametoa maelekezo kwa Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi Wilaya ya Chamwino kuhusu kudhibiti na kuchukua tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa Corona ( COVID - 19).

Maelekezo haya aliyatoa jana  Machi 18, 2020 alipofanya kikao na Kamati hiyo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chamwino.

 Maelekezo yaliyotolewa ni kuwa Viongozi wote katika ngazi ya Wilaya , Tarafa, Kata ,Kijiji na Vitongoji  Wahakikishe  wanatoa Elimu kuhusiana na Ugonjwa huu kwa Wananchi, pamoja na kusimamia maelekezo yote yanayotolewa na Serikali kuhusiana na Ugonjwa huu.

 Vile vile amewaelekeza Viongozi wa Taasisi  zikiwemo, Shule na Vituo vya kutolea huduma za Afya , Viongozi wa Dini wahakikishe pia wanatoa Elimu kwa Watu wanaowahudumia na kusimama maelekezo  yote yanayotolewa na Serikali kuhusiana na Ugonjwa huu, ikiwa ni pamoja na kuhimiza suala la  kunawa Mikono kwa kutumia maji safi tiririka na sabuni. Pia amesema kila mmoja kwa Imani yake amuombe Mungu ili Ugonjwa huu usifikie hatua ya kuondoa uhai wa ndugu zetu.

“ Kila Taasisi iweke  maji safi tiririka na sabuni kwa ajili ya kunawa Mikono  na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya  na Mkurugenzi watashirikiana kuahakikisha kila Taasisi inatekeleza Maagizo haya yote. “

Aidha ameelekeza kuwa Wananchi waepuke Mikusanyiko ambayo siyo ya lazima ili kujikinga na maambukizi.

Mkuu wa Wilaya ameelekeza pia wamiliki wa vyombo vya Usafiri kama daladala wanunue dawa za kutakasa mikono kuhakikisha wanawapaka  abiria kabla   ya kuingia kwenye  vyombo vyao vya usafiri  na wakati wa kushuka pia  na hivyo hivyo  ifanyike kwa  wamiliki wa Nyumba za kulala wageni  kwa wageni wanaolala kwenye  nyumba zao.

Amewataka wamiliki wa Nyumba za kulala wageni  wafuatilie  na kutoa taarifa iwapo atatokea Mgonjwa  mwenye ugonjwa wa Corona (COVID - 19) .Aliongeza  kuwa kuna umuhimu wa kufanya uhakiki wa wageni wote wanaoingia katika nyumba zao  za kulala wageni na kuendelea  kuwahimiza kujikinga kwa wale ambao wako salama.

Aidha Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa Watendaji wa Kata,Vijiji na Maafisa Tarafa  kusimamia  maelekezo yote yaliyotolea na kutoa taarifa katika ngazi ya Wilaya  kila Wiki na muda wowote zitakapohitajika  na aliomba kila mmoja kuona wajibu wa kutoa taarifa pale inapohitajika.

 Mwisho aliomba wadau watakaoguswa wasaidie kutoa mahitaji yanayohitajika katika kuhudumia  wagonjwa wa Ugonjwa huu iwapo watagundulika.

Aliwashukuru Kampuni ya “YAPI MARKEZ” kwa kutoa mabango yanayoelimisha  kuhusu ugonjwa wa Corona.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.