• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Yaweka Mikakati Mbalmbali Juu ya Masuala Ya Lishe, Rushwa, Malaria na Madawa ya kulevya

Imewekwa: October 6th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Chamwino imeweka mipango madhubuti na wezeshi ili kutokomeza suala la lishe duni kwa kuendeleza michakato mbalimbali ya kilimo cha mahindi katika shule za msingi na sekondari  pamoja na kuendeleza bustani za mboga mboga shuleni ili kuondoa janga la utapia mlo.

Taarifa hiyo imetolewa na katibu tawala wa wilaya ya Chamwino Bi. Neema Nyalege wakati akiwasilisha taarifa ya Halmshauri mara baada ya Mwenge wa Uhuru kumaliza ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyokaguliwa katika wilaya hiyo.

Akitoa taarifa hiyo mbele ya hadhara ya wananchi na viongozi mbalimbali waliohudhuria kwenye mapokezi ya mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Chamwino mwaka 2023 Bi. Nyalege amesema kuwa katika mwaka 2022/2023 hali ya lishe kwa watoto chini ya miaka mitano ni kuwa udumavu ni asilimia 0.2.

"Kwa kuzingatia mwongozo wa Taifa wa lishe kwa mwaka 2022/2023 hali ya lishe kwa watoto  ni kama ifuatavyo udumavu ni 0.2 ukondefu ni 0.3 na uzito pungufu ni 0.7 na takwimu hizi zinaashiria kwamba utapiamlo unapungua kwa kasi katika Halmshauri ya wilaya ya Chamwino.

Bi. Nyalege ameongeza kuwa Mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri imetenga kiasi cha shilingi millioni 96,566,000  kwa ajili ya utekelezaji wa afua za lishe  katika ngazi zote ikijumuisha Halmshaur,i Kata na Vijiji.

Aidha amezungumzia suala la mapambano dhidi ya rushwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kupitia njia za hadhara ikiwemo pia kupitia club za shule lengo ikiwa ni kuziba mianya ya rushwa .

Amesema kuwa kwa mwaka 2022/ 2023 TAKUKURU ilipokea malalamiko 76 na kuyafanyia kazi kwa mujibu wa sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa ambapo mashauri 11 yaliendeshwa katika mahakama ya Chamwino na mashauri 7 kati ya hayo yametolewa hukumu.

Kuhusu suala la madawa ya kulenya amesema kuwa jeshi la polisi wilayani Chamwino kwa kufanya misako ya madawa ya kulevya jeshi hilo kuanzia mwaka July 2022 hadi July 2023  lilifanikiwa kukamata bangi kilo 24.0 kete 234 na misokoto 66 ambapo  hadi sasa kesi 5 zimefunguliwa kituoni na watuhumiwa 12 wamefikishwa mahakamani na watuhumiwa wengine 13 bado upelelezi unaendelea.



Sanajri na hayo pia ameeleza hali ya ugonjwa wa maralia katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na kubainisha kuwa kati ya mwaka 2020 hadi 2022 jumla ya wagonjwa 261,345 walipimwa vimelea vya maralia, kati ya hao watu elfu 24,934 sawa na 6.4%  walikutwa na maralia ambapo wote walipatiwa matibabu na kutumia dawa kwa kipindi cha mwaka 2023 mpaka kufikia mwezi Septemba wagonjwa waliopimwa Malaria  8228  na waliogundulika kuwa na vimelea vya maralia ni 302 sawa na asilimia 3.7%.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.