• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Yaweka Mikakati Kuhakikisha Wanafunzi Wanamaliza Mzunguko Wa Elimu

Imewekwa: May 28th, 2025

Ili kuhakikisha wanafunzi wanamaliza mzunguko wao wa shule kuanzia elimu ya msingi hadi kidato cha nne, kikao cha kutathmini usalama shuleni kimefanyika leo tarehe 28 Mei, 2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kikiwa na lengo la kujadili njia sahihi za kumuepusha mwanafunzi na masaibu yatakayokwamisha kumaliza shule.

Mradi wa Mpango wa Shule Salama unaoratibiwa na Wizara ya OR-TAMISEMI chini ya ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO umetekelezwa katika shule 10 ndani ya Wilaya ya Chamwino kwa kutoa mafunzo kwa walimu juu ya namna ya kupambana na changamoto mbalimbali zinazochangia mwanafunzi kutomaliza mzunguko wake wa elimu zikiwemo ukatili, utoro na kukosekana kwa chakula shuleni.

Akizungumza wakati akifungua kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Tito Mganwa amewapongeza Walimu kwa jitihada mbalimbali wanazozifanya kuhakikisha wanafunzi wanakuwa salama katika maeneo ya shuleni.

“Ninapenda kuwapongeza kwa jitihada mbalimbali ambazo mmekuwa mkizifanya kuhakikisha kwamba watoto wetu wakiwa shuleni wapo katika mazingira salama, na katika hili kumekuwa na ushirikiano wa kila mmoja lakini bado jitihada nyingi zinatakiwa”. Alisema Ndg. Mganwa.

Kwa upande wake Mratibu wa Mpango wa Shule Salama (SSP-COO) kutoka Wizara ya OR-TAMISEMI Dkt. Theresia Kuiwite amesema lengo kubwa la mradi huo ni kumsaidia mwanafunzi kumaliza mzunguko wake wa masomo kuanzia shule ya msingi hadi sekondari.

“Malengo ya mradi au mpango wa shule salama ni kuhakikisha wanafunzi wanapoanza shule wanamaliza mzunguko wao wa elimu na kwa sasa sera ya elimu wanatakiwa waende mpaka kidato cha nne, kwahiyo ni kazi na jukumu letu kubwa kuhakikisha wanafunzi hawa wanafika kule”. Alisema Dkt. Kuiwite.

Aidha, kuundwa kwa klabu za shule salama shuleni, kuwekwa kwa mabango ya kupinga ukatili maeneo ya shule, wanafunzi kutoa maoni katika sanduku la maoni shuleni pamoja na upatikanaji wa chakula ni miongoni mwa mikakati iliyowekwa katika shule ili kumuwekea mazingira salama mwanafunzi aweze kuhitimu masomo yake kwa ufanisi.

Je, tuambie wewe na jamii yako unazingatia usalama wa mtoto akiwa shuleni?

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chamwino Yaweka Mikakati Kuhakikisha Wanafunzi Wanamaliza Mzunguko Wa Elimu

    May 28, 2025
  • Wamiliki Mashine Za Kusaga Nafaka Wahimizwa Kufunga Vinyunyizi Vya Virutubisho

    May 26, 2025
  • Mchengerwa Awataka Maafisa Habari Kuhakikisha Wananchi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Miche 350 Ya Matunda Yapandwa Kuadhimisha Kampeni Ya "Mti Wangu Birthday Yangu"

    May 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.