• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Watumishi na Waajiri Waaswa Kuzingatia Sheria Za Utumishi wa Umma

Imewekwa: November 25th, 2022

Timu ya Makamishina wa Tume ya Utumishi wa Umma wamefanya ziara ya kikazi Wilayani Chamwino ikiwa na lengo la kujifunza jinsi Halmashauri inavyotekeleza majukumu yake hususani kwenye ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa miradi ya maendeleo na katika kujifunza huko wataweza kuboresha utendaji kazi wa kazi za Serikali. Ziara hii imefanyika Novemba 24, 2022.

Kabla ya kwenda kutembelea maeneo husika walifanya kikao na menejimenti ya Halmashauri na ujumbe huo ukiongozwa na Mwenyekiti Mhe. Jaji Amisa Kalombora walielekeza watumishi kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria kanuni na taratibu za utumishi wa Umma kwani tume isingependa kuona watumishi wanafukuzwa kazi kwani ni hasara kwa Serikali na kwa watumishi wenyewe.

Aidha aliwaelekeza watumishi kuwa wabunifu katika ukusanyaji wa mapato ili kuongeza mapato na iwapo kunakuwa na changamoto zitatuliwe kwa wakati kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu.

Vilevile alieleza kuwa wamebaini watumishi kufukuzwa kazi kutokana na kifaa cha kielektroniki cha kukusanya mapato(POS) na kutokana na hilo tume imeamua kufanya ziara ili kujifunza kutoka kwa wadau wenyewe.

Waajiri pia waliaswa kuzingatia sheria, kulinda na kuzingatia haki za watumishi na kwa kufanya hivyo hakutakuwa na malalamiko ya watumishi.

Mwenyekiti pia alieleza kuwa wanajua kuna mamlaka za nidhamu ambazo hazitekelezi majukumu yao na kupelekea mashauri ya nidhamu kuanza upya kutokana na kutozingatia taratibu za mashauri ya kinidhamu na kusababisha hasara kwaSerikali. Aoieleza kuwa Tume inawakumbusha majukumu yao na piawanakumbushwa kuwasilisha vielelezo vya mashauri kwa wakati.

Kwa mamlaka ambazo hazijatekelezamaagizo ya tume zimeagizwa kutekeleza maaagizo hayo ndani ya siku 14 kuanzia Novemba 24, 2022.

Pia Mwenyekiti alieleza kuwa tume imebaini bado kuna mapungufu katika kutekeleza na kushughulikia masuala ya utumishi wa Umma kwa baadhi ya waajiri yanayopelekea watumishi kushindwa kujua majukumu yao na kuwakosesha haki watumishi hususani kwa waajiriwa wapya na kupelekea malalamiko yasiyo ya lazima. 

Aliwaasa watumishi kuzingatia viapo vyao likiwemo sualala kutunza siri za Serikali na wanaovunja viapo vyao wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

Watumishi walitakiwa kutofanya kazi kwa mazoea na kwa manung'uniko. Kunapokuwa na mapungufu wawaendee viongozi wao na kuwaeleza mapungufu hayo ili yashughulikiwe.

Katika ukaguzi uliofanyika wa POS na ujenzi wa madarasa wajumbe walilidhishwa na utekelezaji na kuipongeza Halmashauri kwa kazi nzuri na kuwaomba waendelee na ari hiyohiyo.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.