• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkurugenzi Chamwino awapa mwezi mmoja Watendaji kata kuongeza kasi ya ukusanyaji Mapato

Imewekwa: January 7th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino Ndugu Athuman H Masasi, amewaapa mwezi mmoja watendaji kata wa halmashauri ya chamwino kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato ya halmashauri ili kufikia malengo waliojiwekea kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Ametoa maelekezo hayo jana tarehe 6 Januari, 2021 kwenye kikao kazi kilichowajumuisha watendaji wote wa kata 36 zilizopo katika Halmashauri ya wilaya ya Chamwino kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Ndugu Masasi ametoa mwezi mmoja wa Januari 2021 wa kuwapima, na kufikia mwezi Februari,2021 anataka aone matokeo mazuri kwenye ukusanyaji wa mapato yamepatikana.

‘’Natoa mwezi mmoja wa Januari,2021 na kufikia mwezi Februari nataka nione matokeo mazuri ukusanyaji wa mapato yamepatikana,’’alisema Mkurugenzi Masasi.

Ameelekeza pia wahakikishe kamati za mapato za Kata zilizoundwa ambazo wao ndio wenyeviti  zinakutana na kufanya vikao walau mara mbili kwa wiki  na kuwasilisha benki mapato yaliyokusanywa kwa kila wiki.

Kwa Watendaji wa Kata ambao jiografia za Kata zao hazijakaavizuri ametoa maelekezo kwa Afisa Utumishi  kuhakikisha wanaangalia namna ya kuwapatia usafiri wa pikipiki kwa kuzifanyia matengenezo pikipiki zilizorudishwa na watumishi ambazo hazihitaji matengenezo makubwa.

‘’Afisa utumishi angalia namna ya kuzitengeneza Pikipiki zilizorudishwa na watumishi ambazo hazihitaji matengenezo makubwa na kuwapatia Watendaji waliopo kwenye maeneo yenye mazingira magumu,’’ alisema Mkurugenzi Masasi.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amewataka Watendaji wa Kata kuhakikisha wanakaa kwenye vituo vyao vya kazi kwani kuna watendaji wengine hawakai vituoni na kwa kufanya hivyo hawawezi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Ameeleza kuwa kuanzia sasa hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya watakaoshindwa kukaa vituoni.

Kuhusu changamoto ya uchache wa mashine za kukusanyia mapato (PoS) Mkurugenzi Mtendaji ameahidi kushughulikia ambapo atahakikisha ameongeza mashine nyingine walau Thelethini (30)kwa maeneo ambayo hayana mashine hizo.

Vilevile katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji amemuagiza Kaimu Mweka Hazina wa Wilaya Ndugu Musa Luhamu kuhakikisha anashughulikia changamoto zote za ukusanyaji wa mapato zilizowasilishwa na watendaji hao.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chamwino Yaweka Mikakati Kuhakikisha Wanafunzi Wanamaliza Mzunguko Wa Elimu

    May 28, 2025
  • Wamiliki Mashine Za Kusaga Nafaka Wahimizwa Kufunga Vinyunyizi Vya Virutubisho

    May 26, 2025
  • Mchengerwa Awataka Maafisa Habari Kuhakikisha Wananchi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Miche 350 Ya Matunda Yapandwa Kuadhimisha Kampeni Ya "Mti Wangu Birthday Yangu"

    May 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.