• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Vitongoji Vyote Wilaya Ya Chamwino Kupelekewa Nishati Ya Umeme

Imewekwa: February 2nd, 2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko amehaidi kupeleka umeme katika vitongoji vyote katika Wilaya ya Chamwino.

Mhe. Dkt. Biteko ametoa ahadi hiyo leo tarehe 2 Februari, 2025 alipokuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa CCM jimbo la Chamwino wakati Mbunge  wa jimbo la Chamwino na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mhe. Deo John Ndejembi akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025 katika ukumbi wa shule ya sekondari ya wasichana Manchali.

“Mnavyo Vitongoji 355 katika Wilaya yenu tupeni muda tunafanyia kazi tumemaliza kupeleka umeme katika vijiji vyote mlivyonavyo tunahamia kwenye vitongoji, tumeanza na vitongoji 15 baadae tutakuja vitongoji vingine vyote tutavipelekea umeme”. Amesema Mhe. Dkt. Biteko.

Akiendelea kuzungumzia sekta ya Nishati nchini Naibu Waziri Mkuu amesema mwaka 2024 Tanzania iliongoza katika upelekaji wa nishati ya umeme kwa wananchi.

“Niwape habari njema mwaka jana Benki ya Dunia ilitupima Tanzania katika upelekaji wa nishati ya umeme kwa Wananchi Tanzania tuliongoza na ndio maana mmeona mkutano mkuu wa wakuu wa nchi barani Afrika umefanyika Tanzania sio kwa bahati mbaya kwasababu tunatafuta pesa kwaajili ya kupeleka nishati ya umeme kwa watu”. Aliongeza Mhe. Dkt. Biteko.

Aidha, katika mkutano huo pia Mhe. Dkt. Biteko amehaidi kulifanyia kazi suala la ujenzi wa hospitali mpya ya Wilaya ya Chamwino.

“Nataka nikuhakikishie Mhe. Deo Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia mipango yake kwenye sekta ya afya kujenga hospitali za Wilaya na lenyewe tutalichukulia kwa uzito wake nataka niwahakikishie litafanyiwa kazi.”

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.