• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

Imewekwa: May 8th, 2025

Kutokana na hali ya uwepo wa mvua chache iliyoathiri shughuli za kilimo na upatikanaji wa chakula kwa wingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, leo tarehe 8 Mei, 2025 Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Edson Sweti amesisitiza mahindi yatakayoletwa na Serikali ili kuleta nafuu ya bei ya chakula kwa Wananchi kupelekwa katika kata zote 36.

Msisitizo huo ameutoa kupitia mkutano wa Baraza la Madiwani wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024-2025 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Akizungumza wakati anasisitiza jambo hilo ameomba vyakula hivyo vikiletwa vipelekwe katika kata na sio Tarafa ili kuwarahisishia Wananchi wanaotoka mbali na wa hali ya chini kupata kwa urahisi na kuwapunguzia umbali mrefu wa kutembea kufuata vyakula hivyo.

“Tuonaomba vyakula hivyo vikiletwa katika maeneo yetu wasiweke kwenye Tarafa, kuna Mzee anaenda kununua debe moja anatakiwa kutembea kilomita 30 kwenda kuchukua chakula debe moja bodaboda ni shilingi elfu 10 kwa hiyo tutawaumiza”. Alisema Mhe. Sweti

“Tunaomba Serikali iweze kukaa na kufikiria kwa kina sana kuhusu suala la kuleta chakula katika maeneo yetu, itusaidie angalau kwenye kata pale vijiji vitaweza kupunguza safari kutembea masaa matatu mpaka manne hilo naomba nisisitize sana kwa niaba ya Baraza au kama Mwenyekiti wa Halmashauri mahindi haya yakija kwenye kata 36 yaweze kufika ili iweze kuwa rahisi kuwafikia watu wasiojiweza”. Aliendelea kusisitiza Mhe. Sweti.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Chamwino Mhe. George Malima amelipongeza Baraza hilo la Madiwani kwa kuwa la mfano kwa kuwa na umoja na kuendesha mikutano yake kwa weledi.

“Haya yanatokea kwa kuwa kazi zimefanyika na zinaonekana mmeshirikiana na wakuu wa Idara wote mnaimba wimbo mmoja na Waswahili wanasema ndege wafananao huruka kwa pamoja hongereni sana kwa hilo”. Alipongeza Mhe. Malima.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.