• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya Chamwino na Viongozi wa Halmashauri Wakagua Maendeleo ya Ujenzi Mradi wa Boost

Imewekwa: May 15th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Gifty  Isaya Msuya, 15 Mei 2023 amekagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa shule ya msingi mpya yenye mikondo miwili inayojengwa katika kijiji cha Mjelo, unaotekelezwa kwa fedha za mradi wa Boost.

Mhe. Gifty amesema shule hiyo ilikuwa ni shule shikizi iliyojengwa kwa nguvu za wananchi kwa kujenga darasa la awali na darasa la kwanza .

Hata hivyo ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kukipatia kijiji hicho kiasi cha fedha shilingi milioni 490 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 14, ofisi ya utawala na matundu 24 ya vyoo.

“Ndugu zangu wa Mjelo sisi tumekuja kuangalia maendeleo ya mradi ni dhahiri kwamba tangu kipindi cha Uhuru miaka 60 ya Uhuru iliyopita ambapo kijiji hiki kilikuwa kimoja cha Handali na baadae tukagawanyika na kupata Mjelo na Handali, lakini kwa kipindi tangu mimi nimefika kumekuwa na malalamiko kwamba shule ya msingi Handali imeelemewa inawanafunzi wengi, majengo machache, lakini eneo pia ni dogo na malalamiko haya tumekuwa tukipokea kupitia vikao mbalimbali.”

 “Nimeambiwa hapa kuna shule shikizi darasa la awali na darasa la kwanza ambao wanasomea hapa na sisi tukaona katika utaratibu huu ambao Mhe. Rais ametoa fedha nyingi za kujenga madarasa tukaomba kupitia Mbunge wenu, viongozi wa kata, Waheshimiwa Madiwani, wakawasilisha maombi kwamba tupatiwe shule nyingine pacha na sisi tukaona ni wazo zuri, tukaomba fedha hizi TAMISEMI natukafanikiwa kupata milioni 490 katika eneo hili ambapo yatajengwa madarasa 14, ofisi ya utawala, na matundu 24 ya vyoo “, alisema Mkuu wa Wilaya.

Vilevile Mhe. Gifty amewasisitiza wananchi kushiriki katika utekelezaji wa miradi hiyo kwa kujitolea nguvu kazi ili kuhakikisha miundombinu inajengwa kwa ukamilifu.

Alisema wanachi watakaposhiriki itasaidia kuhifadhi fedha nyingine kwaajili ya kukarabati madarasa ambayo yalijengwa kwa nguvu za wananchi.

“Sasa Serikali ya Mhe. Samia Suluhu Hassani inatoa mabilioni lakini katika kutoa fedha hizi haitaki wanachi wabaki nyuma lazima wananchi wajue kinachoendelea lakini washiriki moja kwa moja kwenye kuhakikisha miundombinu hii inajengwa kwa ukamilifu, lakini fedha inayotumika inatumika vizuri na nguvu kazi inatakiwa wananchi wachimbe msingi, wakusanye kokoto, mawe na bahati nzuri tumejaliwa mchanga huku Handali na Mjelo, tukusanye mchanga ili tupunguze gharama za mradi,”

“ Inaonekana hapa wanchi kujitoa ni shida, kwa hiyo wananchi mnapaswa kujitoa ili shule yetu iwe ya mfano. Lazima zifanane isiwe kule kuna madarasa mazuri huku kuna magofu haitopendeza. Tunahitajika tutoe nguvu kazi ili tusiweke hela nyingi kwenye hizi kazi ambazo tunaweza kufanya kwa mikono yetu, ili pesa zielekezwe kwenye vitu vinavyotoka viwandani zaidi.” Alisema.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.