• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kata, Shule Na Walimu Walioibuka Kidedea Kwa Ufaulu 2024 Wajizolea Vitita Chamwino

Imewekwa: May 10th, 2025


Kata, shule na walimu waliyofanya vuzuri katika mitihani ya kitaifa 2024 kwa shule za msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino wamepatiwa tuzo ikiwemo fedha taslimu katika hafla fupi ya kuwapongeza kwa jitihada zao za kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi.


Hafla hiyo ya kuwapongeza na kuwazawadia ambayo ilibeba kauli mbiu “Chamwino Bila D na E Inawezekana” imefanyika Jumamosi tarehe 10 Mei, 2025 katika ukumbi wa Simba Hotel mbele ya mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri na Mdhibiti Ubora wa Shule Wilaya ya Chamwino Ndg. John Balisidya.


Zawadi na fedha hizo zilijumuisha ufaulu katika masomo ya Hisabati, Kingereza, Sayansi, Uraia, Kiswahili, Maarifa ya Jamii pamoja na tuzo kwa wafanyakazi bora ambapo Kata za Buigiri, Msanga na Chamwino ni miongoni mwa Kata zilizoibuka kidedea kwa kuongoza ufaulu.


Akizungumza katika ugawaji wa zawadi hizo Bi. Zaina Kishegwe Afisa Elimu na Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ambao ni waratibu wa hafla na utowaji wa tuzo hizo amewapongeza na kuwaomba walimu kuongeza jitihada ili kuongeza ufaulu na kufuta alama D na E kwa Wanafunzi katika mitihani ya Kitaifa inayofuata.


“Nina uhakika kuwa kwa asilimia 100 kila mmoja akisimama kwa nafasi yake akatekeleza yale ambayo tumekubaliana kuna uwezekano kabisa Chamwino tukafuta kabisa ufaulu wa D na E, na ni naamini Chamwino tukawa na ufaulu wa asilimia 100”. Alisema Bi. Kishegwe.


Aidha, kwa upande wake mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi Ndg. John Balisidya pia amewapongeza walimu hao kwa kufanya vizuri na kuwaomba ambao hawakubahatika kupata tuzo kuhakikisha wanafanya vizuri ili nao waweze kupata tuzo hizo mwaka 2025.


“Kuanzia mwaka 2018 tumekuwa tukienda mjongeo chanya mjongeo huo chanya si unaenda tu peke yake bali kuna watendaji ambao ni nyinyi mnayoifanya kazi hiyo ya kila siku na ni kazi nzito, ngumu lakini hamchoki na hamkati tamaa, hongereni sana”. Alipongeza Ndg. Balisidya.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Kata, Shule Na Walimu Walioibuka Kidedea Kwa Ufaulu 2024 Wajizolea Vitita Chamwino

    May 10, 2025
  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.