• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

"Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

Imewekwa: April 11th, 2025

"Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana", Mhe. Mayanja

Vikundi vya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu Wilaya ya Chamwino wametakiwa kufanya kazi kama vikundi pasipo kutegeana kutekeleza majukumu kama walivyokaa na kuandika andiko la mradi na kulipekeka Halmashauri.

Hayo yamesemwa leo April 11, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja kwenye hafla ya kukabidhi hundi ya mikopo kwa vikundi hivyo yenye thamani ya Shilingi 144,472,000/=

Akitoa mfano amesema kuna wanakikundi walianzisha mradi wa ufugaji wa kuku lakini wakategeana katika kuwahudumia na mwisho wake kuku wote wakafa.

"Kuna kikundi kimoja nafahamu walikuwa wanafuga kuku mkoa mwingine kabisa, wakawekeana utaratibu wa zamu ya kuwapa kuku dawa, kusafisha banda, kuwapa chakula. Siku moja niliwatembelea nikabaini kwamba kikundi kimewaachia ile kazi kama watu wawili, mtu ikifika zamu yake kila siku anatoa udhuru." Alisema Mhe. Mayanja.

"Walioonyesha ushirikiano walikuwa wawili na baadae wale wawili wakaanza kuambizana kwani hii kazi ni ya kwetu binafsi, wakaanza na wao kutegea mwisho wa siku kuku wakafa, mradi ukafa na deni wakawa wanaendelea kudaiwa." Alisema Mhe. Mayanja

Aliendelea kueleza kuwa leo wamepewa mikopo isiwe watakapofanya ufuatiliaji wakute anayeuelewa mradi ni mtu mmoja au wawili, kwani hata wakishindwa kulipa hatua zitakazochukuliwa ni kwa kikundi chote. Hivyo wote wanapaswa kusimama na kuvuka pamoja na malengo ya kikundi kutimia. Wanavikundi mnapaswa kurejesha mkopo ili kuwa na sifa ya kukopesheka kwa wakati mwingine.

Aidha mkuu wa Wilaya ameeleza kuwa mahitaji ya wanaohitaji mkopo huko vijijini ni makubwa kuliko wanaopata mikopo hiyo. Amewaomba wakawe mabalozi kwa kuwa wamepata fedha kutoka Halmashauri kama kuna mtu atajitokeza kwenye maeneo yao akasema hakuna mikopo wawe wa kwanza kujitokeza kutoa ushuhuda.

Amewaasa wawe na nidhamu ya fedha na muda. Wasiende kubadilisha matumizi ya fedha na kupelekea miradi kukwama na hivyo mikopo hiyo kutoacha alama kwenye maisha yao.

Pia amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha mikopo hiyo kutolewa pasipokuwa na riba.

Nao wanavikundi waliopatiwa mkopo wakiwakilishwa na Esaya Jonas, Anna Sospeter na Oscar Ayub kwa nyakati tofauti wamemshukuru Mhe. Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa mikopo hiyo pamoja na Halmashauri na kueleza kuwa mikopo hiyo itawawezesha kujikwamua kiuchumi na kuahidi kurejesha kwa uaminifu ili na wengine waweze kunufaika kama wao.

Naye Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ndugu Godfrey Mnyamale ameelza kuwa fedha za kukopesha bado zipo hivyo wawapelekee habari hizo na vikundi vingine ili watume maombi na baada ya kuhakikiwa na kukidhi vigezo waweze kupatiwa mikopo.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.