• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Dodoma Yazindua Mradi Wa Usambazaji Majiko Ya Gesi Kwa Gharama Nafuu

Imewekwa: January 9th, 2025

Miongoni mwa agenda za Dunia ni pamoja na  utunzaji wa Mazingira na Kila mmoja anao wajibu wa kuhakikisha hali endelevu ya kuhakikisha mazingira yanatunzwa ipasavyo, katika kuunga juhudi hizo Wizara ya nishati kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamezindua mradi wa usambazaji mitungi ya Gesi Kwa Bei ya ruzuku Ili kuwafikia Wananchi wengi zaidi hususani katika Kona zote za Nchi ikiwemo Mkoa wa Dodoma.

Uzinduzi huo umefanyika leo Januari 8, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule katika viwanja vya Ofisi ya Kijiji Cha Chamwino Ikulu, Halmashauri ya Wilaya Chamwino.

Akizungumza na Wananchi walioshiriki hafla hiyo RC Senyamule amesema" ni Maono ya Mhe. Rais kugawa mitungi 16,530 Kwa wilaya 6 za Mkoa wa Dodoma Kwa bei ya ruzuku, haya ni malengo endelevu ya kidunia ya kuhakikisha nishati safi inapatikana Kwa bei nafuu na Kwa urahisi, thamani tuliyopewa na Rais ni kubwa sana.

"Nitoe rai Kwenu Wananchi, nyie mmepewa mitungi hii Kwa bei pungufu ya Sh.20,800 kwaiyo niwaombe mchangamkie fursa hiyo, lakini pia tumieni Gesi hizo kulingana na maelekezo mliyopatiwa hapa na wataalam", amesema Senyamule.

Aidha RC Senyamule amewataka Wananchi kuwa makini na watu wasiowaaminifu na wasiona nia njema ambao watatumia fursa hiyo Kuwatapeli kupitia vitambulisho vyao vya taifa na kujiingizia fedha kinyume na taratibu.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja ametoa rai Kwa Wananchi kuchangamkia fursa ya ruzuku ya majiko  hayo na kuahidi kuwa Wilaya hiyo watakuwa mabalozi wazuri wa Nishati safi ambapo kuyatimiza hayo wameanzisha kampeni ya "nitunze nikutunze" ambayo inahamasisha Kila kaya kupanda miti kuanzia mitano nakuendelea.

Naye kaimu Meneja REA Bw. Emmanuel yessaya amesema mradi huo unagharimu zaidi ya million  813 na mitungi hiyo ya kampuni ya 'lake gas' inauzwa Kwa Bei pungufu ya 50% ambapo mtungi Wenye Gesi utauzwa Kwa Sh. 20,800 pekee na zaidi ya mitungi laki nne itasambazwa nchi nzima.

Hayo yamejiri ikiwa utekelezaji wa adhma ya Rais wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kuwa ifikapo 2030 zaidi ya 80% ya watanzania kutumia nishati safi na kuepukana na Matumizi ya nishati chafu.

Awali Wananchi hao wamepatiwa Elimu juu ya Matumizi sahihi ya Nishati ya Gesi Ili kuepukana na madhara ya kulipuka Kwa Moto kunakotokana na Matumizi yasiyo sahihi ya Nishati, Elimu hiyo imetolewa na Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Dodoma.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.