• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino yaadhimisha Mapinduzi ya Zanzibar kwa kupanda Miti

Imewekwa: January 12th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma leo Januari 12, 2021 imeadhimisha siku ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kupanda Miti katika eneo la pembezoni mwa Hospitali ya Uhuru Wilayani humo ambapo zaidi ya miche 2000 ya miti imepandwa.

Katika Zoezi hilo lililoongozwa na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Bilinith Mahenge ameambatana na viongozi mbalimbali Serikali akiwepo Katibu Tawala wa Mkoa pamoja na viongozi wengine kutoka Ofisi ya Mkoa na Jiji la Dodoma, Mkuu wa Wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya, Mheshimiwa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi na Wakuu wa Idara na Taasis mbalimbali Wilayani Chamwino na wanafunzi wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Akizungumza baada ya zoezi la upandaji miti aliwashukuru wote kwa kazi nzuri waliyoifanya na hususani kwa wanafunzi wa UDOM waliofika Ofisini kwake na kuomba kupanda miti eneo la Hospitali ya Uhuru ikiwa ni kuunga Mkono juhudi za Mheshimiwa Rais ambapo amewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa Hospitali hiyo.

Aliwaomba wanafunzi wafikishe salamu zake kwa Mkuu wa Chuo kwa kuwaruhusu kushiriki katika zoezi hilo.

Mkuu wa Mkoa ameomba zoezi hilo liwe endelevu na lisisubiri tu siku za sherehe. ‘‘Naomba zoezi hili liwe endelevu na si kusubiri siku za sherehe peke yake,’’ amesema Mkuu wa Mkoa.

Aliongeza kuwa tunao wajibu mkubwa wa kupanda na kuitunza miti hii, ili kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi yanayosababishwa na hewa ukaa inayozalishwa kutokana na viwanda pamoja na shughuli nyingine za kibinadamu.

‘‘shughuli za kibinadamu zinapoongezeka zinaleta mabadiliko ya tabia ya nchi,hivyo ni lazima tuyatunze mazingira yetu na  kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kupanda miti’’ amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha aliongeza kuwa watazidi kuwaomba wanafunzi wa UDOM wasaidie kupanda miti kwenye maeneo mengine watakayoyapanga. Aliomba tupande miti tuwaandalie vizazi vijavyo mazingira mazuri kama sisi tulivyoikuta misitu iliyopandwa na mababu zetu.

Baada ya zoezi la upandaji miti wanafunzi wa UDOM walikwenda kujitolea Damu katika Hospitali ya Uhuru kwa ajili ya kusaidia wagonjwa watakaokuwa na uhitaji wa kuongezewa damu.

Wanafunzi wa UDOM wakijitolea damu katika Hospitali ya Uhuru Wilayani Chamwino.

Na ofisi ya TEHAMA - Chamwino

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.