Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imeibuka kidedea na kuwa mshindi wa jumla kwa Halmashauri isiyokuwa na madeni, Halmashauri inayotumia vyanzo mbadala kuagiza bidhaa za afya, Halmashauri kinara katika matumizi ya mfumo wa MSD Customer Portal na Halmashauri inayowasilisha maoteo yake ya bidhaa za afya kwa wakati na kupatiwa tuzo.
Tuzo hizo zimetolewa na MSD katika kikao cha wadau na wateja wa MSD wanaohudumiwa na kanda ya Dodoma ambapo inahusisha Halmashauri zote za mkoa wa Dodoma, Singida na Halmashauri ya Kiteto, kilichofanyika mei 09, 2025 mkoani Singida.
Kutokana na ushindi huo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Dr. Eusebius Kessy ameipongeza na kuishukuru timu nzima ya menejimenti kwa ushirikiano wao na kusema kuwa bila wao hayo yasingeweza kupatikana.
"Niwapongeze timu kwa kazi kubwa tunayofanya pamoja kama timu na kutuheshimisha kila mahali. Pasipo ushirikiano wenu tusingeweza kuyapata haya." Alisema Dr. Kessy.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Ndg: Tito Mganwa na menejimenti wameipongeza Idara ya Afya kwa Ushindi huo walioupata.
Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
Sanduku la posta: 1126 Dodoma
Simu ya Mezani: 026 296 1511
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz
Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.