• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wakulima Wahimizwa Kuunda Vyama Vya Ushirika Ili Kunufaika Na Mfumo Wa Stakabadhi Ghalani

Imewekwa: July 9th, 2025

Wakulima Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino wahamasishwa kuunda vyama vya ushirika ili waweze kuuza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani kwa ajili ya kujiongezea kipato.

Wito huo umetolewa leo tarehe 9 Julai, 2025 katika kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ya Chamwino ambacho kiliongozwa na Mwenyekiti na Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Pia wito huo umetolewa kufuatia manufaa makubwa yaliyoletwa na mfumo wa stakabadhi ghalani katika minada miwili iliyofanyika katika kata ya Dabalo mwezi Juni 2025 ambapo Wakulima wa zao la Ufuta walijipatia takribani shilingi milioni 605, hivyo kuleta chachu ya kuundwa kwa vikundi vya ushirika katika maeneo mengine ili wakulima waweze kunufaika.

Akihimiza kuundwa kwa vyama vya hivyo vya ushirika Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mh. Janeth Mayanja ameitaka Halmashauri kuhamasisha na kuanzisha vyama vya ushirikika hasa maeneo yanayolimwa zao la ufuta ili wakulima waweze kunufaika.

“Halmashauri ianze uhamasishaji na kuanzisha vyama vya ushirika kwenye maeneo unapolimwa ufuta ili msimu unaokuja pia ufuta huo uuzwe kwa mfumo wa stakabadhi ghalani kama ilivyofanyika hapo Dabalo”. Alihimiza Mh. Mayanja.

Pamoja na hilo Mhe. Mayanja amekemea tabia za baadhi ya Wafanyabiashara kupotosha Wakulima juu ya kutumia mfumo wa stakabdhi ghalani ili kuwapotezea fursa Wakulima ya kujipatia kipato kwa lengo la kunufaisha maslahi yao.

“Hawa Wakulima tuna kazi kubwa ya kuwajengea uwezo huyu mfanyabiashara wa mazao hapa katikati ukimwambia twende kwenye mfumo wa stakabadhi ghalani hayupo tayari kwasababu yeye alikuwa ananunua shilingi 1000 halafu ufuta hapa unauzwa shilingi 2400 anaona dili kwake limekufa kwahiyo huyu mfanyabiashara ndiye anayeeneza sumu kwa wakulima”. Alikemea Mhe. Mayanja

Sanjari na hilo, ametoa wito pia kwa kutolewa kwa elimu kwa Wananchi kulima mazao yanayostahimili na kuendana na hali ya hewa katika maeneo yao ili kuepusha Wananchi kutumia gharama kupanda mazao ambayo hayatostawi katika maeneo yao.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Tito Mganwa amewahakikishia wafanyabiashara kuwa Halmashauri itaharakisha ujenzi wa machinjio ya mifugo katika Kata ya Chamwino ili Wananchi waweze kupata kitoweo kilichobora na salama kwa matumizi yao.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wakulima Wahimizwa Kuunda Vyama Vya Ushirika Ili Kunufaika Na Mfumo Wa Stakabadhi Ghalani

    July 09, 2025
  • Watumishi Chamwino Wapigwa Msasa Mfumo Wa e- Utendaji

    July 08, 2025
  • Manejimenti Chamwino Yapokea Mradi Wa Tuinuke Pamoja

    July 02, 2025
  • Katibu Tawala Chamwino Ahimiza NGO'S Kutoa Taarifa Za Utekelezaji Wa Shughuli Zao

    June 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.