• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU: WATUMISHI WA UMMA MSIKATE TAMAA

Imewekwa: February 11th, 2021

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma wasikate tamaa kwa vile mishahara mipya haijatangazwa na badala yake amewasihi waendelee kuchapa kazi kwani maslahi yao yanaendelea kuboreshwa.

“Nitoe wito kwa watumishi wa umma, wasikate tamaa kwa sababu mishahara mipya haijatangazwa, kikubwa waendelee kuwasilisha hoja zao kupitia mabaraza yao ya wafanyakazi,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Alhamisi, Februari 11, 2021) wakati akijibu swali la mbunge wa Konde, Bw. Khatibu Said Haji (ACT-Wazalendo) katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu bungeni jijini Dodoma. Mbunge huyo alitaka kujua ni lini wafanyakazi wa Tanzania watapandishiwa mishahara na kuboreshewa maslahi yao.

“Serikali inayo dhamira na inaendelea na suala la kuboresha maslahi ya watumishi wa umma. Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani ilibaini kwamba ukitangaza kupandisha mishahara, unawaumiza watu wengi wakiwemo wakulima, wafugaji na wavuvi kwani gharama za bidhaa hupandishwa haraka sana.”

Amesema Serikali imejifunza kuwa inapotangaza hadharani kuhusu kupandishwa mishahara, imekuwa inasababisha ugumu wa maisha kwani huduma nyingine kwenye masoko ama usafiri wa mabasi zote zinapanda.

Waziri Mkuu amesema maslahi ya watumishi wa umma hayapo kwenye mshahara peke yake bali pia yanaboreshwa kwa kupunguza kodi na kuwapandisha madaraja. “Mheshimiwa Rais Magufuli alisema kupandisha mshahara kwa sh. 20,000 au 30,000 haina tija kwa mtumishi bali kupunguza kodi kunamsaidia zaidi mfanyakazi,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Serikali inapotwaa ardhi ni lazima pafanyike tathmini ili kujua eneo husika lina thamani gani kulingana na mali zilizopo iwe ni nyumba, mazao au kiwanda.

Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum (CHADEMA), Bi. Esther Matiko kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu bungeni. Mbunge huyo alitaka kujua ni kwa nini tathmini zinazofanyika hazikamiliki na wananchi wakalipwa fidia ili waende sehemu nyingine wakaendelee na shughuli zao.

Waziri Mkuu amesema ardhi ni mali ya Serikali lakini kila mtu anapaswa kuwa na hati ya kutambulisha matumizi ya ardhi anayoimiliki. “Kila mtu anapaswa kuwa na hati ya kubainisha ardhi anayoimiliki ni ya kitu gani, iwe mashamba, kujenga nyumba au kiwanda,” amesema.

“Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kama unalo eneo ambalo wananchi wana malalamiko, ni vema uyafikishe kwa viongozi wa eneo husika ili utaratibu wa fidia ufanyike,” amesema.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.