• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali yalegeza Masharti ya Mikopo ya asilimia 10

Imewekwa: February 27th, 2021

Na Mwandishi wetu, Chamwino

SERIKALI, imelegeza masharti ya kukopa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa Halmashauri kwa Vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu ilikuviwezesha vikundi vingi zaidi kukopa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Nne wa Maafisa Maendeleo Jamii.

Waziri Jafo amesema kuanzia tarehe 26 Februari, 2021 Serikali imerekebisha na kutoa kanuni mpya ambazo zimechapishwa kwenye gazeti la serikali ilizianze kutumika na kuwa moja ya kigezo kilicholegezwa nikupungua kwa idadi ya wanakikundi.

‘Kigezo cha kuwa na idadi ya watu kumi kwa vijana na wanawake na watu watano kwa walemavu, kwa muda mrefu kumechangia kwa baadhi ya watu waliokubaliana na malengo yaliofanana kushindwa kuungana’.

‘Kanuni mpya zinasema kwa vikundi vya vijana na kinamama wakipatikana watano kikundi hicho kinaweza kukopesheka lakini tumeenda mbali zaidi kubadilisha kanuni kumwezesha hata mtu mmoja mwenye ulemavu anaweza kupewa mkopo, haya ni mapinduzi makubwa’ amesema Waziri Jafo.

Amesema kuanza kutumika kwa kanuni hizi mpya kutatoa fursa kwa vikundi vingi kuwa na sifa ya kupata mikopo hiyo.

Waziri Jafo amesema kuwa katika eneo lingine ambalo limeimarishwa ni suala la urahisishwaji wa ufuatiliaji wa mikopo kwa serikali kutenga fungu kulingana na ukopeshaji wa kila mamlaka.

‘Kuanzia sasa kanuni mpya zinaelekeza kwa kila Halmashauri kutenga kiasi cha fedha ili kuwawezesha Maafisa Maendeleo Jamii kufanya tathimini na ufuatiliaji wa mikopo iliyotolewa’

Akifafanua zaidi, Waziri Jafo amesema kwa Halmashauri ambazo mapato yake ya ndani hayazidi shilingi Bilioni moja katika kila marejesho Idara ya Maendeleo ya Jamii itatengewa shilingi laki tano wakati Halmashauri ambazo mapato yake ni zaidi ya shilingi bilioni moja zimeelelezwa kutenga kati ya milioni moja na shilingi milioni moja na nusu kwa mwezi kwa ajili ya ufuatiliaji.

Aidha kwa Halmashauri ambazo mapato yake yapo kati ya shilingi bilioni tano na kuendelea amesema Idara ya Maendeleo ya Jamii ipatiwe shilingi milioni tano kwa ajili ya tathimini na ufuatiliaji.

Sambamba na maboresho hayo, Waziri Jafo ameziagiza mamlaka za serikali za mitaa, kuhakikisha wanawahusisha wataalamu wa maendeleo ya jamii kwenye miradi yote inayotekelezwa katika eneo husika kuanzia hatua za awali.

Amesema kutokana na umuhimu wa Maafisa Maendeleo Jamii kama wahamasishaji wa jamii kwenye shughuli za maendeleo, ameziagiza Mamlaka za Serikali za mitaa kuwashirikisha wataalamu wa kada hii katika miradi yote inayotekelezwa.

Kufuatia kauli hiyo ya Waziri Jafo, akizungumza kwa niaba ya Maafisa Maendeleo Jamii wenzake, Rais mpya wa Chama hicho Angela Kiama, amesema wamepokea kwa furaha mabadiliko ambayo serikali imeifanya katika kanuni.

‘Tatizo lilikuwepo mathalani kwa walemavu, unaweza kukuta mlemavu mmoja katika eneo anashindwa kupewa mkopo kwa kigezo cha kuwataka wawe kikundi, kwakweli tunaishukuru serikali kwa kuliona hili nakufanya maboresho kwenye kanuni hizo’ amesema Kiama.

Maafisa Maendeleo Jamii hao waliokutana kwa siku tatu kutathimini hali ya utendaji kazi sambamba nakuwachagua viongozi wa Chama chao.

Mkutano Mkuu wa Maafisa Maendeleo Jamii, ni wanne tangu kuanzishwa kwa Chama hicho mwaka 2017, na ulikuwa na kauli mbiu ‘Maafisa Maendeleo ya Jamii Nguzo Muhimu kufikia Uchumi wa Viwanda’ na umewashirikisha maafisa wa kada hiyo kutoka serikallini na taasisi binafsi.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.