• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WEKENI MKAKATI WA KUFANYA MAZOEZI

Imewekwa: May 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amewahimiza wananchi kuweka mkakati wa kufanya mazoezi kwa lengo la kuweka sawa miili yao ili kukabiliana na magonjwa ambayo yamekuwa yakiwa kumba mara kwa mara.

Mhe. Senyamule ameyasema hayo leo Wilayani Chamwino kwenye mkutano wa kwanza wa sayansi za afya uliondaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa lengo la kuhakikisha afya bora kwa wote.

"Lakini wapo ambao hata hayo mazoezi ya kutembea hawafanyi kwahiyo niendelee kutoa shime suala la mazoezi liwekewe mkakati nakumbuka tuliwahi kukaa kwenye kikao tukaazimia maafisa ustawi wa Jamii kwenye kila kata watafute eneo wawawekee wazee walau mara moja kwa wiki kuwakutanisha ili wafanye mazoezi yanayoendana na umri wao",amesema.

Pia amewaomba wananchi kuendelea kuhamasishana ili wajitokeze kwenda kupima Afya zao na kujua mapema juu ya kile kinachowatatiza kabla ya ugonjwa haujawa mkubwa na kuweza kutibiwa mapema.

Aidha, ameongeza kuwa elimu ya afya inapaswa kuendelea kutiliwa makazo kwani ni nyenzo muhimu katika kupambana na magonjwa yasiyo ambukiza na kuimarisha ustadi wa kimaisha huku akiongeza kuwa wananchi hawana budi kuzingatia ulaji ulio bora.

"Elimu ya Afya ni nyenzo muhimu katika mapambano dhidi ya Magonjwa yasiyoambukiza, elimu ya mabadiliko ya mtindo wa maisha hususani ulaji unaofaa, umuhimu wa mazoezi na aina zake, madhara ya utumiaji wa tumbaku na mazao yake, unywaji hatarishi wa pombe na njia zake na kuepukana na msongo wa mawazo unaosababisha magonjwa yasiyo ambukiza yatafundishwa na wataalam waliobobea katika maswala haya", ameongeza.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa chuo Kikuu cha Dodoma Prof. Albino Tenge amesema kuwa moja kati ya lengo kuu la mkutano huo ni kutimiza lengo la tatu la maendeleo endelevu la umoja wa mataifa linalolenga maisha yenye afya bora na ustawi kwa watu wote.

"Tuna ushahidi wa kutosha kwamba magonjwa yasiyo ambukizwa kama vile moyo, kisukari, shinikizo la damu la juu na magonjwa mengine yameongezeka duniani kote na athari zake wote tunaziona na zimekuwa kubwa zaidi hasa katika nchi za kipato cha chini na kati",amesema.

Ameongeza kuwa katika zoezi hilo wanategemea kuwafikia watanzania 1000 mpaka 1793 lengo likiwa ni kuongeza ufahamu kwa wananchi kuhusu magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa kushirikiana na Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dodoma kimendaa siku mbili za Uchunguzi wa kibingwa Bure unaofanyika katika Hospitali ya Uhuru iliyopo wilayani Chamwino mkoani Dodoma.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.