Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TARURA yashiriki kutoa elimu ya kinga dhidi ya maambukizi ya UKIMWI

Imewekwa: May 28th, 2021

Na Brian Machange- Chamwino

Ofisi ya TARURA Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imewezesha kutoa elimu ya kinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kwenye mradi wake wa ujenzi wa barabara unaotekelezwa katika Kata tatu za Idifu, Nghahelezi na Manzase Wilayani Chamwino kwa kipindi cha robo ya tatu 2021.

Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Kenneth Yindi alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli zilizotekelezwa na kamati ya kudhibiti ukimwi kwa kipindi cha robo ya Januari hadi Machi 2020/2021,kwenye kikao cha Baraza la madiwani kilichofanyika wilayani Chamwino.

Amesema kuwa Halmashauri hiyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kutekeleza majukumu yake ya mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ili iweze kufikia malengo ya sifuri tatu ifikapo mwaka 2030, 

Halmashauri ya wilaya ya Chamwino kwa kushirikiana na Tume ya kudhibiti ukimwi na shirika lisilo la kiserikali la TAYOA limesambaza jumla ya makasha 508 yenye kondom 10,200 kwenye kata 25 za wilaya hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu mwaka 2021.

Mheshimiwa  Yindi ambaye pia ni diwani wa kata ya Buigiri alitaja kata ambazo zilizosambaziwa makasha hayo ya kondom ni pamoja na Nhinhi, Mlowa Bwawani, Manzase, Chiboli, Fufu, Loje, Mpwayungu na Nghambaku.

Kata zingine ni Chinugulu, Huzi, Manda, Chilonwa, Membe, Dabalo, Itiso, Segala, Chamwino, Buigiri, Msanga, Manchali, Handali, Igandu, Nghahelezi, Mvumi Misheni na Mlowa Barabarani.

Makamu huyo alisema kuwa kwa upande wa huduma ya tiba kwa magonjwa ya ngono na kinga kwa ajili ya kuzuia na kusambaa hutolewa katika vituo vipatavyo 70 vilivyopo katika Halmashauri na kwa kipindi cha miezi mitatu jumla ya wateja 2050 walijitokeza huku wanawake wakiwa 1050 na wanaume 1000.

Hata hivyo alisema kuwa bado kuna changamoto kwa kamati za kudhibiti UKIMWI ndani ya kata kutowasilisha kikamilifu taarifa za utekelezaji za kila robo mwaka kutokana na kutotilia mkazo athari za maambukizi ya virusi.

Aidha kwenye kikao hicho, Madiwani viti maalumu wameiomba Halmashauri hiyo pamoja na taasisi zisizo za kiserikali kuhakikisha wanasambaza pia kondom za kike ili kulingika kundi hilo na maambukizi ya virusi vya UKIMWI kama ilivyo kwa wanaume.



Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wamiliki Mashine Za Kusaga Nafaka Wahimizwa Kufunga Vinyunyizi Vya Virutubisho

    May 26, 2025
  • Mchengerwa Awataka Maafisa Habari Kuhakikisha Wananchi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Miche 350 Ya Matunda Yapandwa Kuadhimisha Kampeni Ya "Mti Wangu Birthday Yangu"

    May 22, 2025
  • Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Ashiriki Zoezi La Kuboresha Taarifa Kwenye Daftari La Kudumu La Wapiga Kura

    May 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.