• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali Yaendelea Kuhakikisha Wanawake Wanawezeshwa Kiuchumi

Imewekwa: March 8th, 2024

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kuchukua jitihada mbalimbali za kuhakikisha kuwa Wanawake wanapata fursa na haki sawa katika nyanja zote za kijamii.

Hayo yamebainishwa leo Machi 8, 2028 na Mhe. Kassima Majaliwa aliyewakilishwa na Mhe. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia, Wanawake na makundi maalumu kwenye viwanja vya shule ya Msingi Chinangali 11 Wilaya ya Chamwino wakati wa maadhimisho ya kilele cha siku ya Wanawake Duniani kwa Mkoa wa Dodoma.

"Katika kudhihirisha hili, Serikali imeendelea kuwezesha Wanawake kupitia Mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi ambapo, jumla ya Shilingi Bilioni 743.7 zimetolewa na kunufaisha watanzania 6,064,957, wakiwemo Wanawake 3,288,186 sawa na asilimia 54 na wanaume 3,556,359 sawa na asilimia 46.

"Serikali itaendelea kuimarisha upatikanaji wa mikopo ili kuwawezesha Wanawake kupata mitaji ya biashara. Hii ni pamoja na kuimarisha mikopo isiyokua na riba ya asilimia 10 inayotolewa kwa makundi maalumu kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa." Amesema Mhe. Majaliwa

Akitoa salamu za Mkoa kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule amesema Dodoma unafanya maadhimisho haya kila mwaka kwani mwaka 2023, yalifanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa ambapo Wanawake zaidi ya 10,000 waliweza kushiriki.

Aidha, ameongeza kuwa, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mambo mengi kwenye Mkoa wa Dodoma kwani Serikali ya Mkoa Ina viongozi Wanawake kwenye kila nyanja kwa asilimia kubwa. Hii inawapa shime Wanawake kugombea ngazi mbalimbali za uongozi Serikalini.

Sanjari na hayo, uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Jinsia na maendeleo ya Wanawake ya mwaka 2023 umefanyika.

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani (SWD) yalianza mwaka 1911 kufuatia maandamano ya Wanawake wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Marekani kupinga mazingira duni ya kazi kama vile ukosefu wa huduma za kijamii na uwepo wa vitendo vya unyanyasaji katika ajira.

Tanzania kama ilivyo kwa mataifa mengine ilianza kuadhimisha siku hii mwaka 1997. Mwaka 2005, maadhimisho yameendelea kufanyika kila mwaka kwa ngazi ya Mkoa na yale Kitaifa hufanyika kila baada ya miaka mitano (5). Maadhimisho ya mwaka huu yameongozwa na kauli mbiu inayosema "Wekeza kwa wanawake: Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na ustawi wa Jamii".

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.