• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Naibu Waziri wa Kilimo aagiza kufanya Maboresho Mradi wa Umwagiliaji Zabibu Chinangali

Imewekwa: January 9th, 2021

Na Brian Machange - Chamwino

Naibu Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Hussein Bashe, ameagiza maboresho yafanyike kwenye Mradi wa Umwagiliaji  Zabibu wa Chinangali uliopo  wilayani Chamwino mkoani Dodoma unaosimamiwa na Chama cha Ushirika cha Chabuma AMCOS.

Mheshimiwa Bashe ameyasema hayo hivi karibuni alipotembelea Mradi huo wa umwagiliaji wa Zabibu uliokuwa haufanyi kazi kwa kipindi kirefu ambapo ametoa maelekezo kwa vyombo vyote vinavyohusika na mradi huu kuhakikisha unaanza kufanya kazi tena. Amemuagiza Mrajis wa Vyama vya Ushirka kufanya Semina katika chama hiki cha Chabuma AMCOS ili kutoa elimu juu ya ushirika na kutoa elimu ya Stakabadhi Ghalani kwa wanaushirika na wakulima kwa ujumla.

Naibu Waziri amewaagiza Mkurugenzi wa Wilaya ya Chamwino, Ndugu Athuman Masasi na Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege, kuwaandikia barua wanachama wote wenye mashamba yao kwenye mradi huo kuyasafisha ndani ya siku thelathini (mwezi mmoja), na atayekiuka na kutosafisha shamba lake ndani ya siku hizo basi anyang’anywe shamba lake.

“Tume ya Umwagiliaji kesho walete wataalam watakaobadilisha mfumo wa mitambo kutoka kutumia umeme kwenda kutumia nguvu ya jua (solar system); na naitaka Tume ya Umwagiliaji kuweka kambi hapa shambani kwa gharama zake ili iweze kufanya uchunguzi wa vifaa vinavyotumika kwenye umwagiliaji katika mashamba haya,” amesema Mhe. Bashe.

Naibu Waziri wa Kilimo ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI), ndani ya miezi minne kuleta miche ya Zabibu kwa wanachama wenye mashamba yao kwenye mradi huo na amewataka wakulima katika kipindi cha kusubiri miche waweze kufanya kilimo cha Karanga kwenye mashamba hayo.

Aidha, Mhe. Bashe amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Bi. Vumilia Nyamoga, kusimamia kurejeshwa kwa transfoma lililoondolewa kwenye mradi huo na ameagiza TAKUKURU kusimamia kurejeshwa kwa Shilingi milioni 150 zilizokopwa na Chabuma AMCOS kutoka ALKO Vintage.

“Hii ni mara ya mwisho kuwainua tena, Serikali haitaingilia mradi wowote mtakaouharibu kwa makusudi; tumeshaweka mkakati mzuri wa kibiashara na tumetafuta mnunuzi yuko hapa, Alko vintage ambaye ameahidi kununua Zabibu zote zitakazolimwa. Vilevile, Benki ya CRDB tutakaa nao meza moja tuone namna ya kuweza kulipa deni la Shilingi bilioni 2.4 wanazodai kwa Chabuma AMCOS, nawahakikishia wakulima hakuna atakayeumia na deni hili,” alisema Naibu Waziri wa Kilimo.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chamwino Yaweka Mikakati Kuhakikisha Wanafunzi Wanamaliza Mzunguko Wa Elimu

    May 28, 2025
  • Wamiliki Mashine Za Kusaga Nafaka Wahimizwa Kufunga Vinyunyizi Vya Virutubisho

    May 26, 2025
  • Mchengerwa Awataka Maafisa Habari Kuhakikisha Wananchi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Miche 350 Ya Matunda Yapandwa Kuadhimisha Kampeni Ya "Mti Wangu Birthday Yangu"

    May 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.