• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Yaweka Mikakati Kupandisha Ufaulu Elimu ya Msingi

Imewekwa: January 19th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Gift Isaya Msuya amefanya kikao kazi na walimu wakuu na Maafisa Elimu Kata leo Januari 19, 2023 chenye lengo la kuweka mikakati itakayowezesha Wilaya kufanya vizuri kitaaluma kwenye elimu ya msingi.

Kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo alipokuwa akifungua kikao amepongeza juhudi zilizofanyika mwaka jana kwa kuendelea kulinda nafasi waliyokuwa nayo pamoja na kuongeza ufaulu kwa asilimia 0.8.

Mkuu wa Wilaya pia ametumia kikao hicho kutoa maelekezo mbalimbali yakiwemo masuala ya uandikishaji wa wanafunzi wa awali na darasa la kwanza ambao wanaonekana kurandaranda kwenye maeneo ya biashara na kilimo wafuatiliwe na kuchukua hatua ili waende shule. Aliendelea kusema kuwa walau kufikia mwezi wa pili wafikie asilimia 100 au ikipunguwa sana iwe asikimia 90.

Vilevile aliongelea kuhusu maadili ambapo kumekuwa na masuala ya ulawiti kwa wanafunzi, walimu na wanafunzi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi kwa wanafunzi kulawitiana. Alieleza wazazi wanaamini malezi ya watoto wao yanatoka kwa walimu.

Alisisitiza pia suala la utoaji wa chakula cha mchana shuleni ambapo bado liko chini. Aidha alizungumzia suala la maelekezo ya mkoa kuhusu upandaji wa miti ambapo alwataka walimu kuwasimamia wanafunzi kila mmoja apande mti na kuusimamia hadi utakapokuwa na akimaliza shule walisishwe wanaobaki.

Vilevile alielekeza kila shule na kila kata ianzishe vitalu vya miti na miche hiyo itakapokuwa tayari igawiwe kwenye taasis za Serikali ili ipandwe na kila kaya pia itapaswa kuapanda miti mitano na kuanzia mwezi wa tatu watapita kukagua.

Suala la shule kuwa chafu, alielekeza walimu wawasimamie wanafunzi kufanya usafi.

Suala la kusaini mikataba alieleza kuwa mkataba ni sheria hivyo kwa kushindwa kutekeleza yaliyomo kwenye mkataba watachukuliwa hatua. Aliendelea kueleza kuwa mitihani ya kila mwezi ndio itakayotumika kupima matokeo( performance appraisal) watakaofanya vizuri watapongezwa na watakaofanya vibaya watapewa bendera nyekundu wakapeperushe kwenye shule zao.

Aliwaomba wawe tayari kujifunza na kufanya mabadiliko. Vilevile wawe na utayari wa kupokea maelekezo ya viongozi. Wajifunze kwa wengine waliofanikiwa hawataonekana wajinga kwa kufanya hivyo.

Mkuu wa wilaya pia aliahidi kusimamia haki za walimu na watumishi wengine kama waziri wa TAMISEMI alivyoelekeza lakini alisisitiza haki iendane na wajibu.

Katika kikao hicho wajumbe walipitia na kujadili kuhusu mpango kazi wa Mkoa kuhusu elimu ya msingi pamoja na mpango mkakati maalum wa Wilaya kwa ajili ya darasa la saba.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Msisitizo Watolewa Mahindi Ya Bei Nafuu Yanayotolewa Na Serikali Kupelekwa Kila Kata

    May 08, 2025
  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.