• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chamwino Yafanya Mjkutano wa mwaka wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali

Imewekwa: August 31st, 2022


Halmashauri ya wilaya ya Chamwino imefanya mkutano wa mwaka na mashirika yasiyo ya Kiiserikali yanayofanya kazi wilaya ya Chamwino mapema wiki hii kwenye ukumbi wa Serikali ya kijiji uliyopo Chamwino.

Mgeni rasmi wa kikao hicho alikuwa Afisa Tarafa wa Tarafa ya Chilonwa ndugu Mohamed Mfaki ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Gift Isaya Msuya.

Katika hotuba yake mgeni rasimi aliwapongeza washiriki wote kwa kuitikia wito wa kushiriki mkutano huo wa mwaka wenye kauli mbiu "Uendelevu wa mashirika yasiyokuwa ya Kiserkali: Wadau tuwajibike."

Alieleza pia Serikali ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inatekeleza majukumu mbalimbali kuhakikisha changamoto katika jamii zinatatuliwa kwa wakati. Hivyo kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya Kiserikali itaharakisha kufikiwa kwa matokeo tarajiwa.

Vilevile alieleza kuwa mamlaka za Serikali za mitaa zinawajibu wa kusimamia mashirika yanayofanya kazi katika maeneo yao. Lengo la mkutano huo ni kukutanisha mashirika yote yasiyo ya Kiserikali yanayofanya kazi katika wilaya ya Chamwino kwa pamoja ili waweze kujadiliana masuala mbalimbali katika kuboresha huduma kwa jamii na kuendelea kushirikiana kutekeleza miradi na programu mbalimbali hasa katika ustawi wa wanancni.

Alieleza kuwa Serikali inaendelea kusisitiza nia yake ya kuendelea kujenga na kuboresha mazingira wezeshi kwa masirika yasiyo ya Kiserikali nchini kufanya kazi kwa ufanisi na kuchochea maendeleo ya wananchi katika maeneo ambapo afua za mashirika zinatekelezwa.

Pia alisema Serikali inatambua wazi mchango na kazi kubwa wanayoifanya katika kuisaidia Serikali ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Aidha alieleza kuwa mkutano huo ni fursa muhimu kujadiliana masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kujengeana uwezo kuhusu sheria na kanuni zinazoongoza mashirika yasiyo ya Kiserikali na Serkali pia kufahamu changamoto na shughuli zinazofanywa na mashirika ili kuwa na uelewa wa pamoja

Alitoa wito kwa mashirika kuendelea kuimarika kwa kufanya kazi kwa ufanisi na uzalendo, kufuata sheria na kanuni zake kwa manufaa ya maendeleo ya wilaya ya Chamwino. Serikali ipo tayari kupokea maoni na changamoto kupitia baraza la Taifa la mashirika yasiyo ya Kiserikali yaani NaCONGO na wilaya ya Chamwino inao wajumbe watatu ambao waliwachagua.

Alisisitiza suala la kuwepo kwa uwazi na uwajibikaji kwenye mipango yaoya kila mwaka hususani kuanzia kwenye kata na vijiji wanakotekeleza miradi. Alieleza pia si jambo jema kwa ofisi yake kupokea malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya sheriakutoka pande zote za Serikali na mashirika. Alishauri kila mmoja atumie kwa usahihi mifumo ya kiuratibu iliyowekwa kisheria na kanuni zake.

Alishaurikila shirika kuwa na mpango mkakati wa kupata fedha za kutekeleza shughuli zake kwa jutumia rasilimali za ndani zilizopo kuliko kutegemea wafadhili kutoka nje ya nchi. Hiyo itasaidia mashirika madogo kutofutiwa usajili kwa kushindwa kutekeleza miradi, kutoa taarifa za utekelezaji na kutolipa ada ya mwaka.

Aidha alieleza kuwa kumekuwa natabia ya mashirika yasiyo ya Kiserikali mengi kujikita maeneo ya mijini ambayo mara nyingi hayana changamoto kubwa kama ilivyo kwa maeneo ya vijijini. Alitoa wito kuwa ni vizuri washirikishwe wataalamu ngazi ya wilaya ili washauri wapi kuna uhitaji wa miradi.

Alisisitiza mashirika hayo kushirikiana na wataalamu wa Serikali ngazi zote kiwilaya ili kuhakikisha kunaiuwa hakuna mwingiliano wa na migongano ya kiutendaji na kiuratibu katika kufikia azima ya kuwaletea wananchi maendeleo kwa uharaka.

Katika mjutano huo mambo mbalimbali yaliweza kujadiliwa ikiwemo utendaji kazi wa mashirika hayo, mafanikio na changamoto wanazopitia. 

Pia wajumbe walijadili na kuweka mikakati itakayoboresha utendaji kazi wao hususani katika suala la utoaji wa taarifa za utendaji wao wa kazi.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Chinangali II Wapokea Neema Ya Mradi Wa Milioni 261

    May 06, 2025
  • "Fanyeni Kazi Kama Vikundi Pasipo Kutegeana" Mhe. Mayanja

    April 11, 2025
  • TSC Chamwino Yawapatia Tuzo Walimu Kwa Ufaulu Mitihani Ya Kitaifa

    March 27, 2025
  • Wakuu Wa Shule Wapatiwa Mafunzo Ya Mfumo Wa NeST

    March 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.